Na
Juhudi Felix
Karagwe
Watu saba wakazi kijiji cha Rugarama kata ya Ihanda wilaya karagwe wamefariki
dunia baada ya kulipukiwa na kitu kilichosadikiwa kuwa ni bomu.
Tukio hilo
limetokea October 30 mwaka huu majira ya saa nne asubuhi katika eneo la kijiji
hicho.
Jeshi la polisi wilayani humo limedhibitisha kutokea kwa
tukio hilo ambapo limewataja marehemu hao kuwa ni Eladius Robert(15),Fenius
Frank(miaka 3 na miezi 6),Faraja Frank(mwaka 1 na mwezi 3)na wengine waliopoteza
maisha kuwa ni Scatus Kamali(15),Nelson Lphonce(14)Edger Gidion(14) na mmoja
ambaya jina lake ambayae halikufahamkika mara moja(17).
Inadaiwa kuwa marehemu walikuwa wanaokota vyuma chakavu
katika eneo la kijiji hicho kwa ajili ya kuuza kwa wafanyabihara wanatoka inchi
jirani,ambapo pia imeelezwa kuwa watoto wane kati ya hao wanatoka katika
familia moja.
Mmoja wa wazazi wa marehemu Frank Robert(35) alieleza kuwa
marehemu hao walikuwa wamehiti darasa la saba September mwaka huu na walikuwa
wakiokota vyuma chakavu kwa ajili ya kuuza
“jana hao wanangu ambao ni mrehemu wana kitu kama kidumu asubuhi walikuwa wanakusanya vyuma vyao
kwenda kuuza ndio ghafra nilisikia mlipuko mkubwa”alisema Robert.
Kwa upande wake Ruteni Col Benedict Kitenga ambaye ni mkuu
wa wilaya ya kyerwa na mtaalamu wa kutegua mabomu amekili vifo hivyo
kusababishwa na bomu(defencive hand grunet)ambapo amewataka wananchi kuwa na
tahadhari wanapoona kitu ambacho si cha kawaida katika maeneo yao.
Kitenga alisema wilaya za karagwe na kyerwa zikom mpakani na
nchi za Rwanda,Burundi,Uganda na kongo,kuwa wananchi wajihadhari na wageni
wanaoingia ili kulinda amani ya nchi yao na maisha yao.
No comments:
Post a Comment