KKKT DAYOSISI YA KARAGWE
HOSPITALI TEULE YA
WILAYA – NYAKAHANGA
RISALA KWA MGENI RASMI WAZIRI MKUU WA JAMUHURI YA MUUNGANO WA
TANZANIA KATIKA KILELE CHA JUBILEI YA MIAKA 100 YA HOSPITALI NYAKAHANGA TAREHE
02/09/2012.
Mheshimiwa, Mgeni rasmi,
Mheshimiwa Raisi Mstaafu, Dkt Benjami W. Mkapa
Mheshimiwa, Baba Askofu Dayosisi ya Karagwe,
Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa wa Kagera
Waheshimiwa wakuu wa wilaya kutoka mkoa wa Kagera,
Mh. Mkuu wa Wilaya ya Karagwe,
Mh. Makamu M/kiti wa Halmashauri ya wilaya, Karagwe
Mh. Mkurugenzi, halmashauri ya wilaya ya Karagwe
Waheshimiwa viongozi wa serikali,madhehebu ya dini,vyama vya
siasa,taasisi na mashirika binafsi na ya umma,
Waheshimiwa wageni waalikwa, mabibi na mabwana.
1. UTANGULIZI
Mheshimiwa Mgeni rasmi, jumuiya ya Nyakahanga hospitali inayoongozwa
na KKKT Dayosisi ya Karagwe kwa
ushirikiano na serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, tunapenda
kukushukuru kwa dhati kukubali mwaliko wetu, na kuungana nasi katika siku hii
ya kilele cha jubilei.
Mheshimiwa Mgeni rasmi, maadhimisho haya yanayofikia kilele chake leo
tarehe 2/9/2012 yalianza tangu Jumapili ya tarehe 26/8/2012 kwa ibada maalum
iliyofanyika hapa uwanjani na kuongozwa na Mhashamu Baba Askofu Dkt. Benson
Bagonza na siku ya Jumatatu tarehe 27/8/2012 mpendwa wetu Mkuu wa Wilaya ya
Karagwe Mh. Darry Ibrahim Rwegasira alizindua rasmi huduma zilizotolewa hapa
uwanjani kwa juma nzima.
Mh. Mgeni rasmi, katika juma hili la maadhimisho hospitali kwa
kushirikiana na wadau mbalimbali wa ndani na nje ya nchi tumekuwa tukitoa huma
bure za uchunguzi wa afya na ushauri wa kitaalam kwa wananchi waliotembela
vibanda vilivoandaliwa.
Huduma zilizotolewa ni pamoja na:
Ø Huduma za elimu ya afya
Ø Huduma za uchunguzi wa
magonjwa ya kisukari, moyo na shinikizo la damu
Ø Huduma za upimaji wa virusi
vya ukimwi
Ø Huduma za elimu na uchunguzi
wa saratani ya matiti
Ø Uhamasishaji wa uchangiaji
wa damu
Wananchi wengi wamepewa ushauri wa kitaalam juu ya afya zao na wale
walioonekana kuhitaji tiba zaidi wameandikiwa kwenda sehemu husika kwa
uchunguzi zaidi na tiba kama ifuatavyo:
·
General consultations
731
·
Diabetic clinic – klinik ya Kisukari 263
·
Upimaji wa VVU 2036
(66 sawa na asilimia 0.03 wamekutwa na maambukizi ya VVU, utaratibu wa
kuwapatia huduma zaidi umeelekezwa kwao)
·
Waliochangia damu 19
·
Uzazi wa mpango 73
·
Upasuaji (surgeries) 14
·
Uchunguzi wa saratani ya matiti 108 ( kati ya hao 11
waligundulika kuwa na matatizo na kufanyiwa utaratibu ya uchunguzi zaidi,
wengine wawili walikutwa na majibu na kufanyiwa upasuaji)
JUMLA YA WANANCHI WOTE WALIOPEWA HUDUMA KATIKA PANGO HUU MAALUM WA
MAADHIMISHO YA MIAKA 100 NI 3134
Mheshimiwa, Mgeni rasmi, msingi wa huduma ya tiba katika hospitali ya
Nyakahanga ulianzishwa na wamisionari kutoka Misioni ya Bethel, Ujerumani. historia inaonesha kwamba mwishoni mwa mwaka 1912 kituo kidogo cha tiba
kilianzishwa hapa Nyakahanga.
Mheshimiwa mgeni rasmi, kituo hicho kwa wakati huo kilipitia misukosuko
mingi ikiwemo kubadilika kwa utawala wa wakoloni kutoka kwa wajurumani kwenda
kwa waingereza. Pia matukio ya vita kuu ya kwanza na ya pili ya dunia
yaliathiri kwa kiasi kikubwa kituo hicho.
Athari hizo ni pamoja na kukatishwa kwa huduma kwa vipindi fulani lakini
pia kuhama kwa kituo kwenye maeneo ya Bugene na Lukajange, kabla ya kurudishwa
tena hapa Nyakahanga mwaka 1939 chini ya wamisionari waanzilishi.
Mwaka 1953,Kanisa la kiinjili la kilutheri lilichukua rasmi uendeshaji
wa zahanati ya Nyakahanga toka kwa wamisionari ikiwa na uwezo wa kulaza
wagonjwa wapatao 60 tu. Na mwaka huo huo kituo kilipandishwa hadhi na
Hospitali. Mwaka 1953 – 1959 hospitali ilikuwa na majengo 3 na wagonjwa
wachache. Zilikuwepo wodi mbili tu ambazo leo zinajulikana kama wodi B na C
Mnamo mwaka 1965 kulikuwa na haja ya Karagwe kuwa hospitali ya wilaya.
Tarehe 11.2.1965 serikali iliandika barua kuleta maombi kwa Kanisa kuhusu
Nyakahanga kufanya kazi kama hospitali ya wilaya. Ombi hilo lilikubaliwa na ndipo
serikali na Kanisa waliingia kwenye makubaliano ya namna ya kuendesha hospitali
hii ikiwa hospitali teule ya wilaya ya Karagwe.
Mh. Mgeni rasmi, Makubaliano hayo yalitaja wazi wajibu wa kila upande
kuwa, Kanisa (KKKT) litakuwa mmiliki wa hospitali,kuajiri watumishi,kutunza na kuendeleza majengo (capital expenditure) na pia kusimamia
uendeshaji wa shughuli za hospitali, Serikali kwa upande wake itawajibika kwa
kutoa ruzuku ya mishahara kwa watumishi na pesa zote za uendeshaji wa Hospitali
za siku kwa siku (recurrent expenditure).
Mheshimiwa Mgeni rasmi, huduma zitolewazo na hospitali hii ni pamoja na:
Ø Huduma za wagonjwa wa nje.
Ø Elimu na huduma ya afya ya
msingi
Ø Huduma za afya ya uzazi
Ø Huduma ya wakinamama
wajawazito na watoto
Ø Huduma za upasuaji
Ø Huduma na kinywa na meno
Ø Hudma za macho
Ø Huduma za afya ya akili –
mental health
Ø Huduma kwa walio na
maambukizi ya VVU
Ø Huduma za tiba shufaa (palliative
care) na huduma majumbani kwa wagonjwa mahututi (homebased care)
Ø Kliniki ya kisukari
Ø Huduma za uchunguzi kwa
mionzi - diagnostic radiology
Ø Uchunguzi wa njia ya chakula
– endoscopy
Ø Huduma za maabara
Mheshimiwa Mgeni rasmi, hospitali hii inao uwezo wa:
Ø vitanda 224 vya kulaza
wagonjwa,
Ø wafanyakazi wa kudumu 254;
Ø inahudumia wakazi zaidi ya
600,000 toka ndani na nje ya Karagwe.
Ø Wastani wa wagonjwa
wanaotibiwa kwa mwaka;-
o
Wagonjwa wa nje 35,000 – 40,000,
o
waliolazwa 11,000 – 13,000,
o
waliojifungua 3,500 –
4,000 na
o
wanaofanyiwa upasuaji
1,700 – 2,000.
Hospitali hii inasimamia zahanati 4 ambazo zinamilikiwa
na KKKT Dayosisi ya Karagwe.
2. CHANGAMOTO.
1.
Watumishi.
Mheshimiwa Mgeni rasmi, pamoja na
juhudi na kujitoa kwa watendakazi wa hospitali kuhudumia wananchi wenzao,
watumishi hawa wanafanya kazi masaa mengi na kwa kwa kweli wengi wao huwa
hawapati siku za mapumziko wanazozistahili. Hii inatokana na upungufu mkubwa wa
watumishi hasa kwa kada za maafisa tabibu(waganga), wauguzi, wateknolojia na
wateknolojia wasaidizi wa madawa, maabara, mionzi, watoa dawa ya usingizi na
wafamasia.
Mh. Mgeni rasmi, katika hali kama
hii, watumishi wa sekta hii ya afya wanahitaji motisha stahiki ili waweze
kujitoa zaidi zaidi ya sasa katika kuhudumia jamii yenye uhitaji mkubwa wa
huduma za afya na tiba.
Mh. Mgeni rasmi, urasimu na taratibu
zinazobadilika badilika za ajira na kuingizwa watumishi kwenye payrol umekuwa
kikwazo kikubwa kwa juhudi za uongozi wa hospitali kuajiri watumishi
wanaohitajika.
Mh. Mgeni rasmi, watumishi
waliowengi wa hospitali wanaishi kwa mashaka juu ya hatima ya mafao yao ya
kustaafu lakini pia wapo ambao malipo yao ya mapunjo yamekuwa na usumbufu tangu
mwaka 2008. Makato ya fedha zao kwa ajili ya pensheni yamekuwa na utata kwani
imeonekana wengi wanakata fedha toka hazina Dar es salaam lakini haziwekwi
kwenye akaunti zao za mifuko husika.
Mh. Mgeni rasmi, malalamiko ya
watumishi katika sekta ya afya ni mengi, itoshe tu kusema kwamba watumishi wa
hospitali ya Nyakahanga wana imani kubwa na serikali kuwa inayafanyia kazi.
Mh. Mgeni rasmi, kauli mbiu
iliyochaguliwa na watendakazi wa hospitali ya Nyakahanga ni “shabaha yetu ni huduma bora za afya na
tiba”
Kauli mbiu hii mh. Mgeni rasmi
itoshe kukuonyesha wewe, serikali yetu, viongozi wetu wa kanisa na umma wa
watanzania kwamba tumejitoa kufanya kila lililo ndani ya uwezo wetu kufanikisha
shabaha hii.
Mh. Mgeni rasmi, hata hivyo
ikumbukwe kuwa watumishi wa sekta ya afya pia ni watu wenye majukumu ya
kifamilia na kimaendeleo binafsi, hivyo
isichukuliwe tu kuwa hii ni kazi ya wito halafu mtu huyu akashindwa kulisha na
kusomesha watoto wao. Maadhara ya baadaye kwa hali hii ni makubwa. Moja ni watu
vijana wengi kukimbia masomo ya sayansi za tiba. Lakini pia mtumishi huyu pia
atakaposhindwa kusomesha watoto wake ni fedheha kwa jamii na pia kuongeza
vijana wasio na elimu kwenye taifa na hivyo kurudisha nyuma juhudi za maendeleo
kitaifa.
Mh. Mgeni rasmi, changamoto hii ya
watumishi ni kubwa na inaweze kuchukua siku nzima kuiongelea. Itoshe tu
kutambua kwamba bila watumishi wa kutosha na tena wenye ari ya kazi, hata
tungekuwa na majengo mazuri namna gani, hali ya huduma haitafikia malengo.
2.
Miundo mbinu.
Mheshimiwa Mgeni rasmi, miundo mbinu mingi ni ya zamani
hivyo inahitaji ukarabati au kupanuliwa. Upungufu uliopo hasa ni wa vyumba vya
kulaza wagonjwa, vyumba vya ofisi za kufanyia kazi madaktari, nyumba za
watumishi na uchakavu wa mfumo wa maji taka na umeme.
3.
Ruzuku
Mheshimiwa Mgeni rasmi, fedha
zinazotolewa kwa ajili ya ununuzi wa dawa na vifaa tiba toka serikalini ni
kidogo, hazikidhi mahitaji. Hata zile zinazotolewa vifaa na madawa mara nyingi
havipatikani toka kwa msambazaji mkuu aliyeidhinishwa na serikali. Fedha pia zinazotolewa kama “OC” (other charges) ambayo
hutumika pamoja na mambo mengine kugharimia matengenezo ya mitambo na gharama
za umeme ni kidogo, ukilinganisha na makisio/mahitaji halisi
MAKISIO
|
HALISI
|
ASILIMIA
|
MAKISIO
|
HALISI
|
ASILIMIA
|
|
2009/2010
|
2009/2010
|
HALISI V.S
|
2010/2011
|
2010/2011
|
HALISI V.S
|
|
MAPATO
|
TSHS.
|
TSHS.
|
MAKISIO
|
TSHS
|
TSHS.
|
MAKISIO
|
Ruzuku toka Serikalini
|
||||||
-Mishahara
|
1,027,664,280.00
|
662,634,700.00
|
64%
|
991,103,531.60
|
892,076,800.00
|
90%
|
-Vifaa Tiba na Madawa
|
335,661,864.00
|
178,795,996.09
|
53%
|
360,222,482.40
|
200,982,340.86
|
56%
|
- Uendeshaji (OC)
|
467,893,236.00
|
23,911,972.00
|
5%
|
545,948,724.90
|
42,569,300.70
|
8%
|
Mfuko wa pamoja (Busket Fund)
|
237,285,000.00
|
237,355,000.00
|
100%
|
235,360,677.00
|
235,360,677.00
|
100%
|
Vyanzo Vingine
|
364,754,534.00
|
352,015,641.40
|
97%
|
276,900,000.00
|
364,395,545.41
|
132%
|
Jumla ya Mapato
|
2,433,258,914.00
|
1,454,713,309.49
|
60%
|
2,409,535,415.90
|
1,735,384,663.97
|
72%
|
MATUMIZI
|
||||||
Mishahara
|
1,027,664,280.50
|
755,733,276.77
|
74%
|
991,103,531.60
|
897,751,989.50
|
91%
|
Vifaa Tiba na Madawa
|
686,511,604.50
|
291,307,609.00
|
42%
|
694,594,831.90
|
291,053,889.00
|
42%
|
Matumizi Mengine
|
719,083,029.00
|
413,630,427.68
|
58%
|
723,837,052.40
|
484,438,055.59
|
67%
|
Jumla ya Matumizi
|
2,433,258,914.00
|
1,460,671,313.45
|
60%
|
2,409,535,415.90
|
1,673,243,934.09
|
69%
|
4.
Mabadiliko ya mara kwa mara ya sera katika sekta ya Afya
(Health Sector Reforms).
Mheshimiwa Mgeni rasmi, mabadiliko
haya ya mara kwa mara ya sera ya Afya japo lengo lengo ni kuboresha huduma za
afya na tiba, yameleta changamoto nyingi ndani ya hospitali.
Eidha kwa kutotolewa kwa ufafanuzi
wa waraka ama kwa hospitali kutokuwezeshwa kutekeleza kikamilifu yaliyomo
kwenye miongozo mbalimbali.
Mfano:
· Huduma kwa makundi maalum
yenye msamaha
· Sera ya uchangiaji wa huduma
· Miongozo na taratibu za
uapatikanaji wa madawa na vifaa tiba
Waraka wa posho za masaa ya ziada – kugawa watendakazi
5.
Maji:
Mh. Mgeni rasmi, hospitali ya
Nyakahanga inakabiliwa na tatizo la upatikanaji wa maji ya uhakika. Jambo hili
limekuwa mzigo kwa hospitali kwani huchangia kuongeza gharama za uendeshaji.
Kwa mwezi hospitali hulipa kati ya Tsh 600,000 na 700,000 kama gharama za umeme
kwa ajili ya mitambo ya kusukuma maji. Lakini pia tunakabiliwa na uchakavu wa
mitambo hiyo inayohitaji ukarabati wa mara kwa mara na ni wa gharama.
Mh. Mgeni rasmi, hospitali inacho
chanzo cha maji kwenye bonde la Nyakagera, hospitali ni miliki wa chanzo hicho
na inalipa ada ya kila mwwaka kwwa mamlaka ya bonde la ziwa viktoria.
Mh. Mgeni rasmi tatizo linalotukabili kwenye chanzo hiki ni
kutishiwa usalama wa maji na pia kukauka kwani ujenzi wa nyumba za makazi
karibu na chanzo hiki umeshika kasi kubwa.
Mh. Mgeni rasmi, suala la
upatikanaji wa maji safi kwa matumizi ya majumbani ni tatizo kubwa hapa
Karagwe. Hospitalini tumekuwa tukishuhudia madhara haya kwa kupokea wagonjwa
wengi kutokana na kutumia maji yasiyo salama ikiwa wengine hata kupoteza
maisha.
3. MALENGO
Mheshimiwa Mgeni rasmi,tunapofikia
miaka 100 ya kutoa huduma ya afya na tiba hapa Nyakahanga, Dayosisi ya Karagwe
chini ya uongozi wake Baba Askofu Dkt Benson Bagonza, imejipanga kuhakikisha
ile kauli mbiu yetu isemayo “shabaha
yetu ni huduma bora za afya na tiba” inatimia siku si nyingi za usoni.
Mh. Mgeni rasmi, kama ulivyosikia,
changamoto za kutoa huduma bora ni nyingi ila kanisa limejipanga kutafuta
suluhu ya changamoto moja baada ya nyingine
Mh. Mgeni rasmi, moja ya mkakati wa
kukomesha tatizo la uhaba wa watumishi
ni kuanzisha chuo cha sayansi za tiba na afya ambacho kitajumuisha shule za
wauguzi, waganga, wateknologia wa maabara na maafisa afya.
Mh.
Mgeni Rasmi, faida za Chuo hiki ni pamoja na:
a.
Kusaidia kupunguza upungufu wa wataalam wa fani hizo hapa wilayani na nchini kwa
ujumla.
b.
Kusaidia vijana wetu wanaomaliza elimu ya sekondari kupata
elimu ya taaluma kwa gharama nafuu, zingatia mkoa hauna chuo cha waganga, ni
gharama kubwa kwa wazazi kupeleka watoto wao nje ya mkoa kusomea taaluma hio.
c.
Chuo kitatoa nafasi nzuri kwa watumishi waliopo kazini
kuweza kujiendeleza wakingali katika mazingira ya familia zao hivo kupunguza
gharama na usumbufu wa kusomea nje.
d.
Chuo kitasaidia kuongeza ajira hivo kusaidia katika ukuaji
wa uchumi wa mtu mmoja mmoja, familia na taifa kwa ujumla.
Mh. Mgeni rasmi, hospitali pia inayo
mikakati ya kujenga uwezo katika maeneo yafuatayo:-
· Kuendelea kujenga uwezo wa
raslimali watu kwa njia ya mafunzo na ajira.
· Kuboresha majengo ya
hospitali kwa njia ya ukarabati na miundo mbinu ya kisasa kwa kujenga majengo
mapya.
· Kujenga na kuimarisha miradi
endelevu.
· Kujenga jamii ambayo ni
mashahidi wa utukufu wa Mungu kwa njia ya injili.
4. SHUKURANI
Mhe. Mgeni Rasmi, awali ya
yote kwa niaba ya watendakazi wa hospitali teule ya Nyakahanga napenda kuchukua
fursa hii kukushukuru wewe kwa kufika kwako katika kilele cha sherehe hizi za
maadhimisho ya miaka 100 ya huduma hapa Nyakahanga
Shukurani za kipekee ziende
kwa misioni ya Bethel nchini Ujerumani kwa uamuzi wao wa kuanzisha huduma za
afya na tiba hapa Nyakahanga.
Serikali ya Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania kwa miongozo, ruzuku za mishahara, madawa na vifaa tiba na
usimamizi.
Pia kwa maendeleo ya
hospitali hii mpaka kufikia wafuatao ni kati ya wadau wakubwa na wanastahili
shukurani zetu
·
Baba Askofu (mstaafu) Paul Mukuta
·
Baba Askofu (askofu)
Nelson Kazoba
·
Baba Askofu Dkt. Benson Bagonza
·
Mh. Balozi Fredinand Ruhinda
·
Mh. Balozi Sir George Kahama
·
Halmashauri ya wilaya ya Karagwe
·
DANIDA
·
Church of Sweden
·
United Evangelical Mission
·
DMCDD
·
Dan Mission
·
Dan Church Aid
·
ATEGRIS
5. HITIMISHO
Mheshimiwa Mgeni rasmi, kama tulivyokwisha kusema hapo
awali, dhumuni la maadhimisho ya jubilei ya miaka 100 ya Hospitali ya Nyakahanga ni kutaka wananchi na
wadau kufahamu hisoria ya hospitali hii, huduma tunazozitoa, changamoto
zinazotukabili na pia malengo ya baadae ya hospitali katika juhudi zake za
kutoa huduma kwa wananchi kwa kushirikiana na serikali.
Mheshimiwa Mgeni rasmi,
tunapoanzisha chuo, kuna changamoto mbalimbali zinazohitaji nguvu ya pamoja
kati ya Kanisa, Serikali, wadau wa ndani
na nje na wananchi kwa ujumla. Kwa kuzingatia umuhimu wa chuo hiki katika
jamii yetu, kupitia PPP (Public Private Partnership), tunaomba serikali
itusaidie yafuatayo:
-
Tamko la serikali juu ya umuhimu wa chuo hiki ni chachu
inayhitajika kututia hamasa sisi na wadau wengine wa maendeleo
-
Serikali ipunguze urasimu katika usajili wa vyuo kama hivi,
bila kushusha ubora.
-
Kama ilivyo kwa hospitali, serikali iwe mdau katika watakaofundisha
katika chuo hiki
Mheshimiwa Mgeni rasmi, katika
kutimiza malengo tumelenga kukusanya Tshs.1.8 bilioni mpaka sasa tumekwisha
kukusanya 119,402,521, tunakushukuru
wewe kwa kwa harambee uliyoiendesha kwa umahiri mkubwa hapo jana na kuweza
kufikiwa kwa kiwango hicho.
Mh. Mgeni rasmi, tunarudia
kukushukuru kwa ujio wako tukikuomba wewe
pamoja na serikali kutuunga mkono katika juhudi hizi za kuhahkikisha huduma za
afya na tiba zinakuwa bora huku tukiamini kwamba changamoto zote tulizozitaja
na nyingine ulizojionea utaziwakilisha sehemu husika na kupatiwa ufumbuzi .
ASANTE SANA.
Imeandaliwa
na kamati ya Historia
Na
kusomwa na Dr. Andrew Cesari
Mfawidhi
wa Hospitali
0762751335
Nyakahanga,
2/8/2012
No comments:
Post a Comment