Saturday, December 22, 2012

VIONGOZI WA SIASA WALAANI MAUAJI WILAYANI NGARA

Na: JUHUDI    FELIX    NGARA

Baadhi ya viongozi wa vyama vya siasa katika wilaya ya Ngara mkoani kagera wamelaani mauaji ya raia mmmoja  na polisi wawili wa kikosi cha usalama barabarani na kusababisha taflani kubwa ndani ya jamii kwa kukumbwa na hofu ya ya kushindwa kuliamini jeshi la polisi katika utendaji wake wa kazi ya kulinda raia na mali zao.
Katibu mwenezi wa CCM wilayani Ngara Pastori Damiani aliliambia gazeti hili jana kuwa  jeshi la polisi linatumia nguvu katika utendaji kazi zao na kusababisha wananchi kushindwa kulithamini kama ni chombo cha dola
Damiani alisema kuwa serikali pamoja na kuliamini jeshi la polisi kufanya kazi za kulinda raia na mali zao bado jeshi hilo linawanyanyasa raia na kutumia nguvu kwa wavunjaji wa sheria kwa kuwadai rushwa
Alisema mauaji ya raia wa kata ya mugoma na wananchi kuua askari polisi kasha kukiunguza kituo cha polisi  Desemba 15 siku ya gulio yalisababishwa na  askari hao kutumia nguvu nyingi kwa raia huyokutaka kuchukua pikipiki iliyokuwa gereji kwa nguvu kabla ya kumaliza matengenezo na kuikabidhi kwa mteja wake.
“Kama wangeandika maelezo ya makosa ya pikipiki na namba zake kasha wakatoa agizo la mmiliki kufika polisi aidha kituo cha Mugoma au makao makuu wilayani kasha kuendelea na shughuli zao mauaji yasingelitokea”.Alisema Katibu  Mwenezi

Kwa upande wake Mwenyekiti wa chama cha NCCR -Mageuzi Staford Festo  alisema kutokana na mauaji hayo serikali haina budi kujifunza kwa matukio ya mauaji yanayofanywa na jeshi la polisi nchini kwa kukiuka ibara ya 14 ya Katiba ya nchi ya isemayo kila raia ana haki ya kuishi .
 Festo alisema kuwa kitendo cha kuendelea na na mauaji kwa jeshi la polisi kukiuka miiko yao ya kazi ni kusababisha imani ya wananchi kuidharau serikali kwa kuwa haichukui hatua za kinidhamu kwa chombo cha dola kilichopewa mamlaka ya kulinda usalama wa raia
Aliongeza kuwa wananchi licha ya kutumia nguvu na rasilimali zao kujenga kituo cha polisi katika kata mbalimbali wilayani ngara bado wanakasirishwa na unyanyasaji wa vyombo vya dola kukandamiza haki zao
“Kinachosikitisha ni askari hao kufuata wananchi siku za magulio nyakati za kukaribia sikukuu na  kudai rushwa kwa nguvu hasa wanapokamata vyombo vya usafiri kubainika na makosa au kuviendesha bila kuwa na leseni.Alisema

Wakati huo huo mchambuzi wa masuala ya kijamii wilayani Ngara na ambaye ni Mkurugenzi wa shirika la HDT Dr Peter Bujari alishauri kuundwa kwa kamati huru ya uchunguzi wa mauaji bila kuhusisha polisi wanaotuhumiwa kuwa chanzo cha tatizo ili haki itendeke na sheria ichukue mkondo wake
Alisema mkuu wa wilaya ya Ngara costantine kanyasu na mkuu wa jeshi la polisi nchini IGP Saidi Mwemawahakikishe wanahusisha watu maarufu wa kisiasa kidini na kijamii katika kupata ukweli wa mienendo ya utendaji kazi wa polisi na matumizi ya vyeo walivyo navyo katika kulinda raia na mali zao
Aidha Dr Bujali alisema  kamati ya uchunguzi ikikamilika  itolewe  taarifa kwa umma kuhusiana namaamuzi yaliyopendekezwa ili kuondoa manunguniko ya wananchi kulalamikia serikali yao kiutendaji na kutimiza wajibu wake
Alisema wilayani Ngara matukio ya unyanyasaji wa jeshi la polisi kwa raia yamekuwa ya mazoea hasa kwa kipindi cha uongozi wa mkuu wa wilaya Costantine Kanyasu kwani hivi karibuni askari mmoja alimpiga  dereva wa gari la kubeba abiria na kumsababishia maumivu na kulazwa hospitali ya Nyamiaga kwa siku kadhaa.

Hata hivyo mbunge wa jimbo la Ngara kupitia CCM Deogratias  Ntukamazina ametuma salamu za rambi rambi kwa wananchi wa Ngara na kulaani mauaji hayo ya askari wawili wa polisi na raia mmoja kwa kujichukulia sheria mkononi. 
Ntukamazina alisema licha ya kuwa jijini Dares- Salaam kikazi anaungana na wananchi wa ngara kwa maombolezo na kwamba viongozi wa serikali  wafanye uchunguzi wa kina kubaini chanzo cha kuhatarisha amani wilayani Ngara.

No comments:

Post a Comment