Tuesday, January 8, 2013

UPOTOSHWAJI WA HABARI HATARI KWA TAIFA LETU LA TANZANIA WANANCHI WALALAMA



 NA
      JUHUDI    FELIX
 KAYANGA-KARAGWE

Baada ya tukio la askari wawili wa jeshi la polisi kutokea wilayani  Ngara kuwawa na wananchi katika kijiji cha Kasheshe katani Rugu wilaya ya Karagwe  kwa tuhuma za kujihusisha na vitendo vya ujambazi wananchi wameonesha kukerwa na upotoshwaji wa taarifa zilizotolewa na vyombo vya habari vya nje ya mkoa wa Kagera.

Wakichangia mada katika kipindi kilichorushwa na vituo vya Redio  Fadeco fm na Redio Kwaragwe vyote vya hapa wilayani wananchi hao walisema kuwa imefikia hatua vyombo hivyo viache kundanya umma kwani kuficha ukweli huo na kuendelea kutetea  maovu sio njia sahihi ya kutatua tatizo bali ni kuweza kutoa taarifa zilizosahihi ili kuweza kukomesa vitendo viovu hivyo katika jamii.

Akitoa  maoni na ushauri wake Sabbi  Rwazo ambaye ni diwani wa kata ya Kanoni kupitia  tiketi ya CCM akionesha kusikitishwa kwake na upotoshwaji wa habari ulifanywa na vyombo vya nje ya mkoa huu  alisema Taifa limedanganya kupitia chombo cha Umma na kuongeza kuwa amejaribu kuwatafuta kutoa ufafanuzi hawakuweza kupokea simu.

Wakionesha kupoteza imani na jeshi la polisi hapa nchini wamesema matukio ya mauaji dhidi ya raia yanayofanywa na jeshi hilo ndilo chanzo kinachopelekea wananchi kukosa imani na  chombo hicho chenye jukumu la kulinda usalama wa raia na mali zao.Wamesema baadhi ya askari waliingia katika jeshi hilo huku wakiwa mwenendo wao si wa kuridhisha katika jamii amba hawakuwa waaminifu ndio wanachafua jeshilo hivyo na kulitaka jeshi hilo kujisafisha kwa kusema ukweli kama ulivyo.


Wameshauri serikali kubadili mfumo wa utoaji wa ajira kwa jeshi la polisi kuwa  majina ya watakaotaka kuajiriwa na jeshi lolote  lazima yajadiliwe na kujiridhisha kuanzia  ngazi ya jamii kwani kufanya hivyo kutasaidia kupata watu ambao watakuwa na mwenendo mzuri katika  jamii kuliko kutumia njia ambazo hazitambui mtu vema kama ilivyo kwa sasa.

Na hapa ni moja ya msikilizaji  aliyetambulisha kwa jina la Ahumuliza kutoka Omurisimbi kata ya Nyakahanga akitoa maoni na ushauri wake  mfumo wa kuajili vijana wanaojiunga na jeshi lolote ingelikuwa vema kujadiliwa na mikutano ya Vitongoji na vijiji wanakozaliwa maana wao ndio wanawafahamu vema kisha kamati za ulinzi za kijiji na kata zijadili ili kuwasilisha majina kwa mwenyekiti wa ulinzi na usalama wilaya.

 Askari hao  wawili wa jeshi la polisi waliouwawa ni wa wilayani Ngara wameuwawa  katika kijiji cha Kasheshe kata ya Rugu wilayani Karagwe  kwa tuhuma za kujihusisha na wizi wa meno saba ya tembo yenye uzito wa  kilogramu 34 kutoka katani humo.

Askari hao wakiwa na gari aina ya Noha namba hazitambulika kutokana na gari hilo kuchomwa moto na wananchi wenye hasira,  walitokea wilaya ya Ngara wakiwa na mpango wa kununua meno hayo kutoka kwa watu ambao hawajajulikana kuwauzia meno hayo.

Askari hao waliouwawa walijulikana kwa majina  ya E1446 Sajenti  Thomasi Magiro na E 8889 Koplo   Damasi Kisheke wote kutoka katika kituo cha polisi cha wilaya ya Ngara, ambapo pia askari mwingine ambaye amejulikana kwa jina moja la Braighitoni aliweza kuwatoroka wananchi hao na kujisalimisha katika kituo cha polisi Kyanyamisa.

Kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Kagera Philipo Kalangi alifika katika eneo la tukio na kuthibitisha kuwa waliouwawa ni askari na kusema  kuwa uchunguzi wa tukio  hilo unaendelea wa kubaini shughuli ilikuwa imewaleta askari hao pia kubaini  chanzo cha vifo vyao  amewataka wananchi kutojichukulia sheria mikononi.

Ikumbukwe kuwa ni juzi tu tarehe o6.01.2013 askari wawili kutoka wilaya ya Biharamulo mkoani Kagera walikamatwa wakiwa na meno ya tembo sita katika hifadhi ya Taifa Serengeti mkoani Mara wakiwa wameyapakia katika pikipiki waenda kuwauzia watu waliokuwa mjini Mugumu serengeti.

Kamanda wa polisi mkoa wa Kagera  Philipo Kalangi hana budi kukaa na kamati ya ulinzi na usalama mkoa ili kujipanga upya kwa ajili ya kurejesha imani ya jeshi la polisi kwa wananchi ilikuwa imejengeka haswa kwa watangulizi wake  waliofanya vizuri haswa Abdallah  Msika,Tossi na wengine ambao waliweza kuimarisha ulinzi katika maeneo ya pori la Kimisi,Nyakanazi  uzuri wa Kondoo na maeneo mengine mengi hapa Kagera.

No comments:

Post a Comment