Monday, January 7, 2013

Wawekezaji wa mifugo kuondoka ndani ya siku 30 wilayani Ngar



Na
     Juhudi  Felix
UONGOZI  katika wilaya ya  Ngara mkoani Kagera umetoa muda wa siku 30 kwa wafugaji wenye asili ya kutoka nchini Rwanga kuondoka na Ng'ombe wao katika ardhi ya wananchi wa wilaya hiyo kabla hatua za kuwasaka na kutaifisha mifugo hazijachukuliwa
Kauli hiyo imetolewa baada yasiku chache za hivi karibuni  wananchi wa wilaya hiyo  kukumbwa na taharuki ya kukosa usalama kwa kuwepo baadhi ya wafugaji  wenye asili ya Kinyarwanda na wengine kutoka katika wilaya za  mikoa ya  hapa nchini  wanaoingia wilayani humo kwa kuwa na  ngombe wengi  kuwanyanyasa wa zalendo wenye ngombe wachache na kuharibu mazao ya wananchi na mazingira kwa ujumla

Mkuu wa wilaya ya Ngara mkoani Kagera Costantine Kanyasu alitoa kauli hiyo jana katika kikao chake na wafugaji wakubwa na wadogo wa kata za kasulo na Rusumo pamoja na viongozi wa kata hiz katika shule ya sekondari ya Kata ya kasulo ili kuhakikisha usalama wa raia na mali zao unapatikana.
Kanyasu alisema ili kuhakikisha amani na utulivu vinapatikana ndani ya siku 30 viongozi wa vijiji kwa kata zote wilayani Ngara wafanye usajili upya wa kuwatambua wafugaji wageni toka nje ya vijiji vyao na mifugo waliyo nayo na kubaini walio ingia kwa njia halali na walioingia kinyume na utaratibu wa sheria waweze kuondoka mara moja

Alisema kuwa serikali inafanya kazi kwa maslahi ya kulinda na kutetea haki za wananchi na sio kutetea kundi dogo lenye uwezo wa kifedha na kuwanyanyasa wachache kwani kufanya hivyo ni kukiuka haki za binadamu na kukwepa uwajibikaji kwa mujibu wa sharia
Alisema kuwa wahamiaji haramu hata kama walipata vibali vya kuingiza mifugo na muda wao kuisha lazima waondoke na wengi wao zaidi ya asilimia 70 wanaingia kwa mianya ya rushwa kutokana na watendaji wa idara za uhamiaji kufanya kazi bila uadilifu na kwamba kama bado kuna wanaokumbatiwa na wenyeji kamati ya ulinzi na usalama itawasaka na kubomoa makazi yaliyoko kwenye ardhi ya wanachi  ili kulinda mazingira
“Tumechoshwa na kubembelezana na wafugaji wanaojionesha kana kwamba serikali ya Tanzania iko mifukoni mwao na kiongozi atakayekwamisha zoezi hili lazima achukuliwe hatua haraka sana “Alisema Kanyasu
 
Aidha kauli hiyo imetolewa sanjari na kupiga  marufuku viongozi wa vijiji kuwakaribisha wahamiaji wenye mifugo kutoka ndani na nje ya nchi wanaoomba ardhi ya kupata malisho na kusababisha uharibifu wa mazingira na kutishia amani ya wananchi kati ya wakulima na wafugaji wilayani Ngara
Alidai kuwa wafugaji hao wamekuwa na tabia ya kuonea wananchi kwa utajiri wao wa mifugo na kuharibu mazingira huku wakiweka vibarua kuywachungia mifugo yao na wao kuishi nje ya wilaya au kwenye nyumba za kulala wageni
Aliongeza kuwa baadhi ya wafugaji kwa kushirikiana na wanachi wasio wazalendo wakiwemo baadhi ya watumishi wa serikali wasio waaminifu wanaendesha  udalalai wa kuwaita wafugaji wengine na kuwauzia mapori ya kuchungia bila kuhusisha wamiliki wa mapori hayo
 
Katika hatua nyingine  Kanyasu alisema katika kikao hicho kuwa wafugaji wengi wanakimbiza mifugo yao kutoka  wilaya ya karagwe mkoani Kagera na wilaya za mikoa mingine hapa nchini kwa kuletwa na wanachi wasio wazalendo kwa kuwa wameshabaini viongozi wa Ngara hawako makini katika kusimamia sheria
“Wananchi wana huruma sana katika kukaribisha wageni lakini pia elimu ya mazingira hawajaitilia maanani na hasara itakayopatikana kwa kuruhusu mifugo migi kuingia na kusambaza uoto wa asili”
Alisema ili kukabiliana na wimbi la mifugo ni lazima mwenye kutuma maombi ya malisho apewe taarifa ya kumlipia ng’ombe mmoja shilingi 12,000 /- kwa mwaka na baada ya hapo aombe upya kama aneo litakuwepo apewe tena likikosekana aondoe mifugo yake ili kuepukana na usumbufu kwa jamii
 
Baadhi ya wafugaji waliotoa maoni yao walitofautiana kwa kudai kuwa wamepata ardhi kutoka kwa viongozi wa vijiji na wengine kununua kutoka kwa wanachi lakini wanashangazwa kuona tangu waingie wilayani Ngara mwakan 2002  sasa waamuliwe kuondoka
Aidha mmoja wa wafugaji hao Amabilis Episphori alisema katika kupata maeneo ya kuchungia mifugo yao tangu mwaka 2002  walitoa fedha katika vijiji vya kata hizo kuendesha zoezi la kutenga maeneo ya wafugaji katika mapori yaliyokuwa hifadhi ya wakimbizi wa Kinyarwanda 1994 hadi 1996
Episphori alisema kuwa kila mfugaji alitoa fedha kati ya shilingi 2,000 na Tsh 3,000 na kupatiwa risiti na mihtasari ya kijiji iliandikwa na wao kupewa nakala kulisha mifugo yao katika maeneo hayo
 
Kwa upande wake Eustachius Sabasi amesema ili kuhakikisha amani ya wanachi inapatikana kati ya wakulima na wafugaji na kuondoleana vitisho idadi ya ngombe kwa kila mfugaji ipungue na kubaki kati ya 300 au 400 na watakao baki wapelekwe wilaya nyingine tofauti na wilayani Ngara
“Mheshimiwa mkuu wa wilaya kinachosumbua hapa ni viongozi wa ngazi zote kuanzia kitongoji hadi wilaya na idara zake zinazohusika na ardhi mifugo na uhamiaji wanaendekeza rushwa vinginevyo wafugaji wa kigeni leo waondoke tupate amani na mali zetu’ Alisema Sabasi
Wafugaji wengine wamependekeza kulisha mifugo kwa kuilipia shilingi 2000 kila mwaka pamoja na kulipia maeneo ya kuchungia kati ya ekari 10 hadi 15 kwa mwaka shilingi laki moja kwa kila mwenye ngombe zaidi ya 200 na fedha hizo ziwe za miradi ya maendeleo ya kijiji wazo lililopingwa vikali katika kikao hicho
 
Hata hivyo mwanasheria wa halmashauri ya wilaya ya Ngara na wakili wa kujitegemea Sauli Wilson alifafanua kuwa katika sheria ya ardhi ya mwaka 1999 hakuna aliye na mamlaka ya kugawa ardhi zaidi ya ekari 50  kijijini kwani zaidi ya ekari hizo  lazima kupata kibali kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano.
Wilson alisema wanaohitaji ardhi kwa shughuli yoyote lazima kufuata taratibu za kutuma maombi katika serikali za vijiji na kujadiliwa kasha mkutano mkuu wa kijiji kukubali ama kukataa kutokana na sifa ya muombajina kiwango cha ardhi kama kinatosheleza wananchi katika mipango matumizi ya  maendeleo
“Kama mwenye kuomba ardhi na akapewa kasha akaitelekeza bila kuitumia kwa malengo ya maombi yake wananchi wanayo haki kuidai na kuitumia kwa malengo mengine ya maendeleo kwa kumnyanganya aliyepewa bila kusababisha uvunjifu wa mamani bali kwa kufuata taratibu”
Alisema wananchi wanaharibu mazingira kwa makusudi na kwa mujibu wa sheria ya NEMC wanatakiwa kutozwa faini isiyopungua milioni 50 hivyo wakulima na wafugaji wawe makini ikiwa ni pamoja na kulinda hifadhi ya wanyama pori na rasilimali zilizoko kwenye hifadhi hizo
Viongozi hao walifikia tamati ya kikao kwa kauli moja ya kila mfugaji kuwa na ng’ombe wasiozidi 400   na kuacha vitendo vya kutishiana hatimaye kuhatarisha usalama wa wananchi  kwa kutumia uwezo waomkubwa   kiuchumi kunyanyasa wanyonge kwa kuwatishia kufungua kesi mahakamani.

No comments:

Post a Comment