NA
JUHUDI FELIX
KAYANGA-KARAGWE
Mkuu wa mkoa wa
Kagera kanali Fabian Massawe anatarajia kufanya ziara ya kukagua miradi ya maendeleo katika wilaya
ya Karagwe tarehe 8.01.2013
Kwa mujibu wa
taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na
katibu tawala wa wilaya ya KaragweMustafa S.Saidi imebainisha kuwa mkuu
wa mkoa wa Kagera atawasili hapa wilayani
tarehe 8.01.2013 na kutembelea miradi ya maendeleo mbalimbali.
Katika ratiba ya ziara hiyo mkuu wa mkoa ataweza
kupokea taarifa fupi ya
wilaya,kutembelea shule ya sekondari Ndama kukagua ujenzi wa maabara,kukagua
mradi wa umwagiliaji katika kijiji cha Bujara,kukagua mradi wa maji Charuha ,
kukagua mradi wa ujenzi wa chuo cha ualimu Karagwe kukagua
miradi mbalimbali ya kituo cha
Mavuno.
Miradi mingine
atakayotembelea ni pamoja na ujenzi wa bweni la wasichana katika shule ya sekondari
Kiruruma,kukagua kituo cha walemavu
Chabalisa na kukagua ukamilishaji wa mradi wa ujenzi wa zahanati ya Omurusimbi.
Pia katika
taarifa hii ya ziara ya mkuu wa mkoa wa Kagera inaonesha kuwa ataendelea na
ziara katika wilaya ya Kyerwa mnamo tarehe
9.01.2013.
No comments:
Post a Comment