Wednesday, January 6, 2016

ABIRIA WA MV SERENGETI KUTOKA BUKOBA KUELEKEA MWANZA WARUDISHIWA NAULI ZAO NA MELI YAONDOKA NA MIZIGO TU.


Abiria  waliokuwa  wasafiri  na   jioni  ya  leo  kwa  meli  ya  Mv  Sengeti  kutoka  mji wa Bukoba  kwenda  Jijini Mwanza  wamerudishiwa  Nauli  zao  baada  ya  kubainika  injini  iliyoharibiwa  na  nyavu  za  wavuvi  inahitaji   matengenezo   makubwa  ikiwa  jijini  Mwanza.





Ofisa   Mfawidhi  wa SUMATRA   mkoa  wa Kagera  Patrick  Machia  amesema  meli  hiyo  iliyoondoka  jioni  ya  leo  kwenda  jijini  Mwanza  ikiwa  na  shehena   ya  mizigo  pekee.


Kuharibika  kwa  MV  Serengeti  kuna  fanya  huduma  za  meli  kutokuwepo  kati  ya  Mwanza  na  mji  wa  Bukoba kwasababu  meli  ya  Mv  Victoria  ina  kipindi  kirefu  imeharibika  na  wananchi  kwenye  kampeini  za  uchaguzi  wa  mwaka 2010  Rais  Mstaafu  Jakaya  Kikwete  aliwahaidi  meli  mpya  na  katika   kampeini  za  mwaka  2015  walihaidiwa  meli  mpya  sasa  ni  wakati  wakutatua  changamoto  hiyo.

No comments:

Post a Comment