Monday, January 18, 2016

BREAKINGNEWS CCM NAO WATUMBUA MAJIPU NDANI YA CHAMA CHAO KWA MWENDO HUU ULAJI UTAKOMA.


Baraza Kuu la Jumuia ya wazazi ya chama cha Mapinduzi CCM Imewafikisha mahakamani wakuu wa shule zake tatu za sekondari  a,mbazo ni Tegeta ,Tabata na Mwembe two ya Mkoani Iringa.


Mwenyekiti wa Taifa ya jumuia ya Wazazi Abdallah Bulembo amesema wanatuhumiwa kwa ubadhilifu wa zaid ya shilingi bilioni 2.8,huku Baraza pia likibaini matatizo makubwa katika uendeshaji wa shule 15 inazozimilikiwa na Jumuia  hiyo .

Amesema uamuzi huo wa kufikishwa mahakamani kumefikiwa kufuatia ukaguzi uliofanywa na kubaini matumizi mabaya ya Fedha ambayo haiendani  na  hesabu za shule hizo.


Aidha amebainisha kuwa hali ni mbaya katika shule mbili ambazo hakutaka kuziweka wazi ili kujilidhisha kwanza kabla ya kuwabuluza wakuu wake mahakamani.

No comments:

Post a Comment