Wednesday, January 13, 2016

FEDHA ZA KUTEKELEZA SERA YA ELIMU BURE KWA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI TAYARI SERIKALI IMEZIFIKISHA FEDHA HIZO KWA KILA SHULE MKOANI KAGERA






Mkoa wa Kagera tayari umepokea shilingi milioni 810,157,000 kutekeleza sera ya elimu bure kwa shule za msingi na sekondari kutoka serikali kuu na tayari fedha hizo zimeishaingizwa kwenye akaunti za shule zote za msingi 888 na sekondari 190 za serikali kwa kila halmashauri katika wilaya saba za mkoa wa Kagera.

Hayo yalisemwa na Katibu Tawala wa Mkoa wa Kagera Bw. Nassor Mnambila katika Mkutano na vyombo vya habari uliofanyika  Januari 11, 2016 Katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kagera alipotoa ufafanuzi wa mgawanyo  wa fedha zilizoletwa katika mkoa mzima na na jinsi zilivyogawiwa katika kila Halmashauri ya Wilaya mpaka shuleni za msingi na sekondari kwa ajili ya kutekeleza sera ya elimu bure.


Akitoa ufafanuzi wa fedha zilizoletwa Mkoani Kagera Bw. Mnambila alisema shilingi 309,461,000/= zimepelekwa katika shule za msingi 888 ambapo shule 16 kati ya hizo ni shule maalum.  Fedha zilizotajwa hapo juu ni ruzuku ya uendeshaji (capitation grant) kwa kila shule ambapo kila mwanafunzi ametengewa shilingi 10,000/= kwa mwaka, lakini fedha hizo hazikutolewa  kila mwanafunzi katika awamu hii.
Vile vile zimetengwa pia fedha za chakula kwa shule maalum 16 za msingi katika mkoa. Akitolea ufafanuzi wa shule maalum na shule za kawaida Bw. Mnambila alisema shule ya Kashalala iliyopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa ni ya kawaida na tayari imepewa shilingi 354,000/= zilizopo Benki ya NMB Kayanga.


Shule ya Mgeza Mseto ni shule maalum iliyopo katika Manispaa ya Bukoba pia nayo imewekewa shilingi 7,728,000/= katika akaunti yake ya NMB Bukoba,  shilingi 3,042,000/= ikiwa ni ruzuku ya uendeshaji aidha shilingi 7,386,000/= ni fedha ya chakula kwa wanafunzi waliopo katika shule hiyo maalum.

Kwa upande wa shule za sekondari za serikali mkoa una jumla ya shule 190 kati ya hizo 17 ni za bweni na shule zote zimepewa fedha  kwa ajili ya chakula shilingi 1,500/= kwa kila mwanafunzi  kwa shule za bweni, na Serikali imetoa fedha za fidia za ada kwa shule za kutwa shilingi 20,000/= na shilingi 70,000/= kwa shule za bweni. Vilevile imetoa shilingi 25,000/= kwa kila mwanafunzi kwa mwaka kama ruzuku ya uedeshaji.


Kwa uthibitisho wa fedha  kupokelewa shuleni Bw. Mnambila alitoa mfano wa shule ya kutwa ya Nemba iliyopo Wilayani Biharamulo kuwa tayari imepokea shilingi 630,000/= kwa ajili ya ada, shilingi 602,000/=kwa ajili ya ruzuku ya uendeshaji, jumla shule hiyo imepokea shilingi 1,232,000/= kupitia akaunti yake ya NMB Biharamulo.

Kwa shule za bweni, shule ya Sekondari ya Rugambwa iliyopo Manispaa ya Bukoba imepokea shilingi 31,179,000/= kwaajili ya chakula, shilingi 4,897,000/= kwa ajili ya fidia ya ada, na shilingi 1,535,000/= kwa ajili ya ruzuku ya uendeshaji ,  julma shule hiyo tayari  imepokea shilingi 37,611,000/= kwenye akaunti yake ya NMB Bukoba.

Mwongozo wa Matumizi ya Fedha
Kwa shule za Msingi, Fedha za ruzuku ya uendashiji zitumike kununulia vifaa vya kufundishia na kujifuzia lakini isiwe zaidi ya asilimia 30% ya fedha za ruzuku ya uendeshaji. Asilimia 30% ya fedha hizo pia itumike katika ukarabati mdogomdogo, asilimia 20% itumike katika mitihani na uendelezaji wawanafunzi na mwisho asilimia 10% ya fedha za ruzuku ya uendeshaji itumike katika mambo ya utawala shuleni.

Shule za Sekondari, Fidia ya ada ambayo serikali imetoa kwa kila shule badala ya wazazi kuitoa itumike kugharamia mambo ya jumla ya uendeshaji wa ofisi mfano vitambulisho, shajala, mandalio ya somo, ulinzi shuleni, madawa shuleni , uendeshaji wa taaluma( chaki, manila karatasi, michezo, mitihani ya uendelezaji wa wanafunzi mfano majaribi o ya wiki, na mitihani ya moko).


Wito, Katibu Tawala Bw. Mnambila alitoa wito kwa Walimu Wakuu wa shule za msingi na Wakuu wa shule za sekondari kuzingatia miongozo ya matumizi ya fedha hizo kwa  kufuata maelekezo ya serikali na kuacha kuyadharau kama baadhi ya yao ambao bado hawataki kuyafuata ambapo alitangza kumvua ualimu Mkuu wa Shule  Mwalimu Mkuu wa Shule ya Sekondari Bilele Siasa Phocus ambaye ameendelea kutoa fomu yenye gharama kwa wazazi wa wanafunzi wanaojiunga kidato cha kwanza na kusema kuwa maelekezo ya serikali hayatambui.


Mgawanyo wa Fedha kwa kila Halmashauri
Kwa shule za sekondari Halmashauri ya Biharamulo  imepata shilingi 76,525,000/=, Bukoba shilingi 56,462,000/=, Bukoba Manispaa shilingi 122,597,000/=, Karagwe shilingi 39,639,000/=, Kyerwa shilingi 21, 403,000/=, Missenyi shilingi 29, 833,000/=, Muleba shilingi 93,757,000/=, Ngara shilingi 60,480,000/=




Kwa shule za msingi  Halmashauri ya Biharamulo  imepata shilingi 43,161,000/=, Bukoba shilingi 36,704,000/=, Bukoba Manispaa shilingi 27,385,000/=, Karagwe shilingi 37,515,000/=, Kyerwa shilingi 37,967,000/=, Missenyi shilingi 20,115,000/=, Muleba shilingi 69,219,000/=, Ngara shilingi 37,397,000/=








No comments:

Post a Comment