Mahabusu watatu waliokuwa wanashikiliwa katika Gereza la Wilaya ya Karagwe Mjini
Kayanga, wakituhumiwa kwa Makosa Sugu ya ujambazi, Wanatafutwa na Jeshi la
Polisi Wilaya ya Karagwe kwa Kuvunja dirisha la Gereza na kutoroka kwa
kukimbilia kusikojulikana..
Hayo yamesemwa na Mkuu wa Jeshi la Polisi wilaya ya
Karagwe Mika Makanja akizungumuza na
Chombo hiki ofisini kwake kuhusiana na
Kutoroka kwa watuhumiwa hao katika Gereza hilo.
Aidha, Makanja amewataja watuhumiwa hao Waliotoroka kuwa
ni Mbaraka Muhamudu Mwenye umri wa miaka 38, Murushid Athumani miaka 25 na
Muhindini Mtasigwa miaka 35 ambao wote kwa pamoja walikuwa wanahukumiwa kwa
makosa ya ujambazi.
Pia ameongeza kuwa watuhimiwa hao walitoloka Januari 11
mwaka huu kwa kukata nondo ya dirisha la choo na kuwataka wananchi kutoa
taarifa kwa jeshi la polisi pindi watakapo waona watuhumiwa hao, kwakua ni watu
hatari katika jamii.
No comments:
Post a Comment