Na
Juhudi Felix
Micheweni-PEMBA
Wananchi wa
Zanzibar wamesema hawako tiyari kuupinga Muungano watahakikisha wana
ulinda na kuutetea kwa nguvu zote.
Haya
yalibainishwa na mkuu wa wilaya ya Wete mkoa wa Kaskazini Pemba Omar Khamis
Othuman Februari 06 mwaka huu katika
ukumbi wa redio ya jamii Micheweni
wakati akifunga mafunzo ya siku tano
yaliyohusisha wajumbe wa bodi wa redio
za kijamii,wahasibu na mameneja wa redio zote za jamii kutoka Tanzania bara na
visiwani zilizo chini ya mtandao unaofadhiliwa na shirika la UNESCO.
Mkuu wa wilaya huyo alisema kuwa wananchi wa
Zanzibar hawako tiyari kuvunja muungano uliopo badala yake
wataulinda,kuutetea na kuudumisha kwa
gharama kwani muungano huo ni tunu na wanajua umuhimu na faida zake za kuwepo.
Alisema kuwa wao kama Wazanzibari wananufaika mno na
uwepo wa muungano na kusema kuwa
changamoto na kasoro zilizopo zifanyiwe kazi lakini haziwezi kupelekea
kuuchukia muungano na kutaka kuuvunja.
Othuman alisema kuwa
kutokana na kuwepo kwa muungano
kuna wanyamwezi,wamakonde, wasukuma na makabila mengi hivi sasa yanakaa
na kuishi Pemba na Zanzibar kwa ujumla bila kubughuziwa wala kuhojiwa kwani ni
watanzania wote.
Aidha, alikwataka washiriki wa semina hiyo na vyombo vya habari kwa ujumla kuhubili na
kuelimisha wananchi juu ya umuhimu wa kulinda na kutunza muungano na kuwapuuza
wale wenye nia ya kutaka kuvunja muungano kwa maslahi ya binafsi.
Mafunzo hayo ilifunguliwa na mkuu wa mkoa wa
Kaskazini Dadi Faki Dadi pia aliwaasa washiriki hao kuendelea
kutangaza na kuhamasisha wananchi juu ya kulinda na kuheshimu muungano ambao
uliasisiwa kwa lengo la kuleta umoja na
mshikamano.
Hata hivyo washiriki wa semina hiyo walihaidi
kuendelea kuulinda na kuutetea muungano na kudumisha umoja na mshikamano uliopo kwa sasa.
Mafunzo hayo yalikuwa mahususi kwa ajili ya kuzijengea uwezo redio za jamii zilizo chini ya shirika la UNESCO kujitegemea washiriki wamefundisha mchanganua wa biashara (Business Plan) na ujasiriamali lengo ni kuwapatia mwanga na uwezo wa kujiendesha.
Mafunzo hayo yalikuwa mahususi kwa ajili ya kuzijengea uwezo redio za jamii zilizo chini ya shirika la UNESCO kujitegemea washiriki wamefundisha mchanganua wa biashara (Business Plan) na ujasiriamali lengo ni kuwapatia mwanga na uwezo wa kujiendesha.
No comments:
Post a Comment