Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, leo tarehe
11 Januari, 2016 amemtembelea na kumpa pole mke wa Baba wa Taifa, Mama
Maria Nyerere kufuatia kifo cha Mkwewe Leticia Nyerere kilichotokea jana
huko Maryland Marekani alikopelekwa kwa ajili ya kupata matibabu mapema
mwezi huu.
Pamoja
na kutoa mkono wa pole kwa Mama Maria Nyerere nyumbani kwake Msasani
Jijini Dar es Salaam, Rais Magufuli pia amewapa pole wanafamilia
wote na amewaomba kuwa wavumilivu katika kipindi hiki kigumu cha
kuondokewa na ndugu yao.
Msemaji wa familia ya Mwalimu Nyerere Bwana Joseph Butiku amemueleza Rais Magufuli kuwa familia inaendelea na taratibu za kuusafirisha mwili wa marehemu kutoka nchini Marekani na itatoa taarifa baadaye.
Msemaji wa familia ya Mwalimu Nyerere Bwana Joseph Butiku amemueleza Rais Magufuli kuwa familia inaendelea na taratibu za kuusafirisha mwili wa marehemu kutoka nchini Marekani na itatoa taarifa baadaye.
Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
11 Januari, 2016
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
11 Januari, 2016
No comments:
Post a Comment