Diwani wa
Kata ya Ndama
Edward Mpaka ameitaka
kamati ya maji
ya kitongoji cha
Rwamugulusi kuhakikisha inasimamia
kimamilifu huduma ya
maji kitongojini hapo
pamoja na kuangalia
upya uchangiaji wa
kupata maji haswa
kwa watu ambao
wana tape binafsi
waweze kuchangia ili
kuboresha huduma ya
maji.
Mpaka akawataka
pia wananchi wanaofanyashughuli za
kibinadamu ndani ya
eneo ya hifadhi
ya chanzo cha
maji kuacha mara moja
kwani kufanya hivyo
ni hatari kwa
uhai wa maji pia
kuwahimizi kuhudhuria mikutano
wanapohitajika kufanya hivyo.
Nao Wananchi wa Kitongoji
hicho cha Rwamugurusi kata
ya Ndama wilayani
Karagwe Mkoa wa
Kagera wameutaka uongozi wa
halmashari ya wilaya
ya Karagwe kupitia
Idara ya Maji
kushauri kampuni inayojenga
barabara kwa kiwango
cha Lami kutoka Kyaka
mpaka Bugene wilayani
hapa kuhamisha mtaro
wa maji waliouelekeza
kwenye chanzo cha
Maji.
Wakiongea na
mwandishi wa mtandao huu
wakiwa kwenye chanzo
cha maji ambapo
walikuwa wanajitolea kufanya
usafi kwenye kisima
hicho wamesema kuwa
kipindi cha mvua
maji yote ya
mvua hutiririka na
kujaa kisimani humo
na kusababisha kuwa
machafu sana na
kubadilika hadi rangi na kuwa
mekundu.
Kwa upande
wake mwenyekiti wa
Kitongoji hicho Thomasi
Ndyanabo amesema malalamiko hayo
alishayawasilisha kwa uongozi
wa halmashauri na kumuhaidi
kuwa watayafanyia kazi
lakini haoni dalili
zozote za kupatia
ufumbuzi malalamiko hayo.
Amesema kwa
kipindi hiki cha
serikali kupambana na
ugonjwa wa Kipindupindu
ni vema wangelichukua
tahadhari kubwa kulinda
chanzo hicho kwani kupitia
maji wananchi wengi
wanaweza kupoteza maisha
kwani huyatumia kila
siku.
Akizungumzia miundo mbinu
ya umeme kwenye kitongoji
hicho ambacho kipo
kwenye mamlaka ya
mji mdogo wa
Kayanga mwenyekiti huyo
alikuwa na haya
ya kusema.
Hata hivyo wananchi
hao wameonesha kushangazwa
na kufurahishwa na
kitendo cha diwani
wa kata hiyo
ya Ndama kushiriki nao kwenye
zoezi la usafi
wa chanzo cha
maji.
No comments:
Post a Comment