Mwenyekiti wa Vijana CHADEMA wilayani Ngara korokoroni kwa kujeruhi mkewe kwa kisu
Na Shaaban
Ndyamukama Ngara
Mwenyekiti
wa Baraza la Vijana kupitia Chama cha Demikrasia na Maendeleo CHADEMA Wilaya ya
Ngara mkoani Kagera Bw Nestori Mashishanga anashikiliwa na jeshi la polisi
wilayani humo kwa kumjeruhi mke wake kwa kisu kwa kile kinachoelezwa kuwa
ni wivu wa mapenzi
Bw Mashishanga alifanya tukio hilo ijumaa aprili 20 katika mji wa Rulenge
wilayani Ngara majira ya saa tano usiku baada ya kumkuta mkewe jirani na baa ya
Upendo kwa dada yake na kuanza kumshambulia kwa kisu kilichomjeruhi pafu la
kulia na sehemu ya bega la kushoto
Kaimu mganga
mkuu wa Hospitali ya Misheni ya Rulenge
Dr prosper Malya alisema mwanamke huyo
alipofikishwa hospitalini alilazwana alipewa matibabu ya majeraha aliyokuwa
nayo kwa kushonwa sehemu alikojeruhiwa kwa kisu lakini hali ilibadilika kesho
yake baada ya kushindwa kupumua
Dr Malya
alisema kuwa katika kufanya zaidi uchunguzi walikuta damu imevimbia ndani ya
pafu lililopatwa na jeraha la kisu na kulazimika kumfanyia upasuaji ili kuona
kama damu hiyo inaweza kutoka na kuokoa maisha yake na kwa kuwa ni mapema
analazimika kulala na baadaye kufanya mazoezi ya kutembea ili damu iweze
kuzunguka mwili mzima
Akieleza
tukio hilo
katika wodi namba 5 ya Hospitali ya Misheni Rulenge mke wa Kiongozi huyo Bi
Neema Nassibu miaka 24 alisema kuwa alikuwa mtaa wa Upendo kumsaidia dada yake
shughuli mbalimbali na alikutwa na mumewe saa 12 jioni na hakuondoka hadi
nyakati za kulala alipoanzisha fujo za kutaka arudi naye kwake kitongoji cha
Murutambikwa kijiji hicho cha Rulenge
Alisema kuwa
kwa kuwa hawakuwa na maelewano ndani ya nyumba na ni siku nyingi ameshindwa
kuishi naye kwa ustaarabu alimkatalia na ndipo alianza kumshambulia huku akitoa
kisu chake cha kukunja na kuanza kumchoma sehemu mbalimbali za mwili wake na
kumsababishia maumivu makubwa “Kusema ukweli mume huyu nimekuwa naye miaka
mitano lakini ananinyanyasa nimemkuta na watoto wawili wa nje ya ndoa na mmoja
ninamlea lakini tangu tuoane ameshakuwa na watoto watatu tofauti na ndoa yetu
na hana uvumilivu kwa kuwa mimi sijajaliwa kuzaa naye”.AlisemaNeema
Mke wa Mwenyekiti wa Baraza la Vijana
wa CHADEMA Wilayani Ngara Bi Neema Nassibu (24) akiwa wodini private chumba namba tano akitibiwa jeraha baada ya kuchomwa kisu na
mumewe kwa kile kilichoelezwa kuwa ni wivu wa mapenzi
Aidha alidai
kuwa katika kuangushana na kupiga kelele alikuja dada yake na shemeji yake
pamoja na mfanyakazi wa baa kuingilia kati vurugu zao na hatimaye kumkamata
hatimaye kumkimbiza katika hospitali kwa lengo la kupata matibabu
Alisema
kabla ya tukio katika maisha yao ya unyumba
wamekuwa na vurugu za kila mara kuhusu kutoaminiana katika ndoa kila mmoja
akimtuhumu mwenzake lakini mumewe amekuwa akijulikana kwa kukutwa na wake
aliozaa nao na wengine wa pembeni na kumtesa katika familia yao
Wanandoa hao
walioana mmoja wao( Neema )akiwa kidato cha tatu na kuacha shule huku kijana
huyo akiwa anafanya kazi katika mgodi wa Kabanga Nickeli kama mlinzi na
wamekuwa wote mtaa wa murutambikwa kijiji cha Rulenge kwa maisha ya Kupanga na
siku za hivi karibuni mashishanga
aliacha kazi madini na kujiunga na siasa katika Chama Cha Demokrasia na
Maendeleo CHADEMA wilayani Ngara
Jeshi la
polisi kituo cha Rulenge wilayani Ngara limethibitisha kumshilia mwnyekiti huyo
wa BAVICHA Nestori Mashishanga na kwamba
amenyimwa mdhamana kwani anaweza kutoroka maana hali ya mkewe haijaleta
matumaini kiafya atika hospitali ya Rulenge.

No comments:
Post a Comment