Tuesday, December 22, 2015

WATOTO WAWILI WA FAMILIA MOJA WAFA MAJI WAKICHOTA MAJI YA KUTENGENEZEA POMBE.


                     Picha  Maktaba
 
Watoto wawili wa  Familia Moja wa kijiji cha  Kanoni Kata ya Kanoni Wilayani Karagwe Mkoani Kagera Wamekufa Maji Desemba 21 mwaka huu  Kutokana na Ajali ya Kudumbukia  katika Dimbwi ambalo walikuwa wakichota Maji kwa ajili ya kutengenezea Pombe.


Watoto hao wanaofahamika kwa majina ya  shamila Ignatus mwenye miaka 10 ambeye pia ni mwanafunzi wa shule ya msingi Ndama na mdogo wake Kato Ignatus mwenye miaka 7 mwanafunzi wa elimu ya malezi katika shule ya msingi Kanoni.


 Baada ya tukio hilo wananchi wa kijiji hicho wamesema kuwa ndani ya miaka minne watoto sita wamefaliki dunia  kwa kudumbukia katika madibwi na visima ambavyo huchimbwa kutokana na shida ya maji iliyopo kijijini hapo.


Aidha wananchi wa jamii ya Kanoni wameshauliwa kufunika madibwi hayo na miti na kuacha matundu madogo kwa ajili ya kuingiza kifaa cha kuchotea maji pekee ili kuepusha vifo vya watoto kufa maji vinavyo zidi kutokea katika kijiji hicho.




No comments:

Post a Comment