Wilaya ya Ngara
Mkoani Kagera kila
siku inapokea wakimbizi
wa wastini 30
hadi 40 katika
kambi ya Rumasi
baada ya nchi
jirani ya Burundi
kutokuwa na utulivu
wa kisiasa.
Kwa mujibu wa
Mkuu wa wilaya
ya NGara HONORATHA CHITANDA wakimbizi
hao baada ya
kufika kufika idadi
ya wakimbizi 250
husafirishwa kwa mabasi
hadi kwenye kambi
zilizopo Mkoani Kigoma.
Katika hatua nyingine
waziri wa Nishati
na madini Profesa
Sospeter Muhongo ameliangiza
shirika la Umeme
Tanzania TANESCO kufunga
umeme ndani ya
wiki moja katika
kituo cha ushuru
wa pamoja(One Border
Post)kilichopo mpaka wa Rusumo
wilayani Ngara baada ya
kubaini umeme unanunuliwa
kutoka nchi jirani
ya Rwanda.
Katika jengo hilo
lenye ofisi za
forodha ,uhamiaji, na polisi
nguzo za umeme
wa TANESCO ziko mita
moja ambapo ofisa
Forodha Mfawidhi katika
kituo cha Rusumo
Laulent Kagwebe amesema
kuwa makubaliano yaliyopo
kati ya nchi
hizo mbili ni
kununua umeme kutoka Rwanda.

AMANI inatakiwa irejeshwe Burundi, viongozi WA maziwa makuu wanahusika, lakini pia bado rais WA nchi hiyo ana nguvu ya kurejesha AMANI.
ReplyDeleteAmani nchini Burundi itadumu kuwa kitendawili kwani Rais wa nchi hiyo anathamini madaraka kuliko uhai na ustawi wa nchi yake na watu wake. Hivyo, jumuiya ya Kimataifa hasa nchi jirani wanapaswa kuangalia hilo kwa jicho la tatu.
Delete