Sunday, December 20, 2015

ZOEZI LA KUPIGA KURA KUWACHAGUA WABUNGE KATIKA JIMBO LA MASASI NA LUDEWA LAANZA RASMI SAA MOJA YA ASUBUHI HII LAKINI MSHIKEMSHIKE UPO MASASI VIJANA WAGOMA KUPIGA KURA KISA FUATILIA HAPA.BOFYA HAPA


Zoezi  la  upigaji  kura  katika  jimbo  la Masasi  mkoani MTWARA limeanza  leo  asubuhi  kwa  vituo  kufunguliwa  na  wananchi  kufuata  utaratibu  lakini  katika  kituo  cha  MSIFUNI 1  zoezi  lilisimama  kwa  muda  kutokana  na  chama  cha  wananchi  CUF   kumleta  wakala  ambaye  hakuapishwa  na  walipohojiwa  walisema  aliyeapishwa  ameugua  na  ambsye  hakuapishwa  alikataliwa  na  kuleta  wa  CHADEMA  naye  akakataliwa  hivyo  baadhi  ya  vijana  ambao  walikuwa  wamepanga  mstari  wakagoma kupiga  kura  wakitaka  mawakala  wote  watimie.





Msimamizi  msaidizi  wa  uchaguzi jimbo  la  Masasi  SHAIBU DADI    amefika  kituoni  hapo  na  kuwatangazia  waendelee  na  upigaji  kura  na  ufumbuzi  wa  tatizo  hilo  limepatiwa  jibu,katika  kata  ya  NYASA watu  hawajajitokeza  kwa  wingi  badala  yake  anakuja  mmoja  mmoja.

Vikosi  vya  ulinzi  na  usalama  vinapita  mtaani  na  siraha  za  kivita  vikiwemo  vifaru  huko  Masasi  mkoani Mtwara.


Majimbo  ya  Ludewa  na  Masasi  wanachagua  wabunge  wao  leo  kutokana  na  uchaguzi  huo  kutofanyika  oktoba  25  kwasababu  ya  vifo  vya  waliokuwa  wagombe  wa  nafasi  hizo  ambo  ni  Dk Emmanueli Makaid  wa jimbo  la  Masasi  na Deo Filikunjombe  wa  Ludewa.

No comments:

Post a Comment