Friday, January 8, 2016

WACHINA WAWILI WANAOKABILIWA YA UHUJUMU UCHUMI KWA KIASI CHA BILIONI 1.1 WAACHIWA KWA DHAMANA.


 Mahakama  Kuu   kanda  ya  Bukoba  imekubali  maombi  ya  dhamana  ya  raia  wawili  wa China wanaokabiliwa   na  kesi ya  kuhujumu  uchumi  na  kusababisha   hasara  ya  zaidi  ya  shilingi bilioni 1.1  wakati  wa   miundombinu  ya  umeme  kwenye  ujenzi wa  barabara ya  Kyaka -Bugene.


Watuhumiwa  wengine   wawili waliokuwa  Mameneja  wa  TANESCO Wilaya  ya  Karagwe  wataendelea  kukaa  rumande  hadi kesi  hiyo itakapotajwa  tena  Januari 18 ambapo raia  hao  wa China  hawaruhusiwi  kusafiri  nje ya Mkoa  bila  ruhusa  ya Mahakama  na  hati  zao  za  kusafiria zitakabidhiwa  kituo cha  polisi  Karagwe.

Raia  hao  wa China  wamepewa  dhamana  hiyo  baada  ya  kiasi  hicho  cha  pesa  bilioni 1.1 kulipwa mahakamani  hapo  lakini  ikaelezwa  mahakamani  hapo  kuwa  bado wanakesi  ya  kujibu.

No comments:

Post a Comment