Sunday, January 3, 2016
WAFANYAKAZI WA JESHI LA MAGEREZA WASHEREKEA MWAKA MPYA KWA KUWAKUMBUKA WAHITAJI..
Wafanyakazi wa jeshi la magereza Mkuza mjini Kibaha mkoani Pwani wameadhimisha mwaka mpya kwa kuwatembelea na kuwafariji watoto yatima na wagonjwa waliolazwa wodi ya wajawazito wazazi, na watoto ikiwa ni sehemu ya sadaka yao ya kumshukuru Mungu kumaliza salama mwaka 2015 na kuanza mwaka 2016
Katika ziara yao hiyo wafanyakazi hao walitoa zawadi mbalimbali zikiwemo sabuni za kufulia, maji safi ya kunywa,mafuta ya kupaka mwili,mchele, mafuta ya kupikia ,mbuzi, na viatu aina ya YEBOYEBO na bidhaa yenye thamani ya zaidi ya shilingi 800,000
Mkuu wa Gereza la Mkuza Mrakibu mwandamizi wa jeshi hilo SSP Emmanuel Malisa amesema wameona furaha ya mwaka waihamishie kwa watu wenye mahitaji kuliko kura na kunywa tu wakati wapo wahitaji.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)


No comments:
Post a Comment