Na Mbeki
Mbeki
BIHARAMULO
ABIRIA
kadhaa wanasadikika kufariki dunia na wengine tisa kujeruhiwa vibaya baada ya
basi walilokuwa wakisafiria kuteketea kwa moto katika kijiji cha Nyantakala
wilayan Biharamulo mkoani Kagera.
Ajali hiyo
imetokea saa 4:30 asubuhi imelihusisha basi la kampuni ya Adventure lenye namba
T 294 ABD aina ya scania ambalo lilikuwa likitokea mkoani Mwanza kwenda mkoani
Kigoma.
Majeruhi wa
ajali wamelazwa katika hospitali teule ya wilaya ya Biharamulo na kwamba kati
ya majeruhi tisa wawili kati yao akiwe ajenti wa basi hilo Dotto
Tryphone[30]mkazi wa Nyakanazi wamevunjika miguu wakati wakijinasua kutoka
kwenye basi hilo baada ya kushika moto.
Kamanda wa
polisi mkoa wa Kagera,Philip Kalangi alithibisha kutokea kwa ajari hiyo na
kusemakuwa basi hilo ni aina y nisani diseal lenye namba T 293 BDP na kuwa chanzo cha ajari hiyo ni
hitalfu ya umeme sehemu ya injini na kwamaba hakuna kifo hata kimoja isipokuwa
mali za abria na basi vimeteketea kwa moto uchunguzi unaendelea,abria walionusurika walisafirishwa na gari jingine .
Aidha Kwa
mujibu wa mashuhuda wa ajali hiyo wakiwemo majeruhi wamesema chanzo cha ajali
hiyo ni baada ya basi hilo kufika kwenye tuta
la kuzuia mwendo kasi
walishitukia moshi unatokea ndani ya basi kabla ya kushika moto na
kuanza kuteketea.
‘’Basi
lilikuwa kwenye mwendo wa kawaida lakini lilipofika kwenye
bamzi[tuta]tulishtukia basi linashika moto ,tukaanza kuruka,kuna baadhi ya
wenzetu hasa watoto na wazee huenda wameteketea kwenye basi hilo,maana basi
limewaka na kuwa majivu kabisa’’alisema Tryphone.
Akizungumzia
ajali hiyo kwa shida akiwa katika wodi ya majeruhi Tryphone alisema huenda
chanzo cha kulipuka kwa basi hilo kinatokana na hitilafu katika mfumo wake wa
umeme.
Dereva wa
basi hilo ambaye hakutambulika jina lake haijajulikana kama alikimbia au
aliteketea kwenye basi hilo mara baada ya kutokea ajali hiyo.
Mganga mkuu
msaidizi wa hospitali hiyo Gabriel Mashauri amesema amepokea majeruhi tisa na
kwamba saba kati yao walikuwa katika hali mbaya lakini bado wanaendelea
kupatiwa matibabu.
Amewataja
majeruhi waliolazwa katika hospitali hiyo ni Phinihas Elias[37]mwalimu wa shule
ya sekondari Shamaliwa Igoma jijini Mwanza,Pius John[21],Msigwa
Isaya[18]mwanafunzi wa shule ya sekondari Kigoma,Johary Chapa[23]Mkazi wa
Kwimba mkoani MwanKza,Josephina Ngereza[46],Rashidi Mahonda[48] na Eles
Ngereza[60] wote wakiwa wameungua moto sehemu mbalimbali za miili yao.
Waliovunjika
miguu katika ajali hiyo wakati wakijinasua kutoka ndani ya basi hilo
wametambulika kwa majina ya Dotto
Tryphone[30]mkazi wa Nyakanazi na Zainabu Issa ambao wote wamevunjika miguu ya
kushoto.
Dk.Mashauri
alisema hajapokea maiti waliotokana na ajali hiyo
No comments:
Post a Comment