Na:Mbeki
Mbeki
Ngara
Wanafunzi
watatu wa shule ya sekondari ya Mt Alfred ya Rulenge wilaya ya Ngara
mkoani Kagera wamefikiswa katika mahakama ya wilaya hiyo wakikabiliwa na tuhuma za kupanga njama na kuhusika kuchoma moto
mabweni mawili ya shule hiyo Agosti 23 mwaka huu.
Akisoma
mashitaka ya wanafunzi hao mbele ya hakimu mfawidhi wamahakama ya wilaya
ya Ngara Juma Mpuya ,mwendesha mashitaka wa polisi Stividana Webiro
aliwataja washitakiwa kuwa ni Gozibert Godwini ( 21),Wilikimuson Daudi ( 16) na
Rameck Biswalo Gama (18 )wote wakiwa wanasoma kidato cha pili na tatu
katika shule hiyo.
Webiro
alisema mnamo Agost 23 mwaka huu majira ya 2:30 usiku washitakiwa walichoma
mabweni mawili ya Nkurumah katika shule ya Sekondari ya mt .Alfred
Rulenge iliyoko wilayani humo na kuwasababishia wanafunzi wenzao kupata hasara
mbalimbali kwa kuunguliwa na magodoro, mavazi, vitabu, vitanda na
vifaa vinginevyo vya kujifunzia.
Katika kesi
hiyo washitakiwa wote watatu walikana makosa hayo na kurudishwa rumande
hadi kesi hiyo itakapotajwa tena September 18 mwaka huu
Aidha
kufuatia tukio la kuunguzwa mabweni hayo kikao cha bodi ya shule hiyo
kimefanyika na kubaini thamani ya hasara iliyojitokeza ambapo
majengo ya shule ,mali za wanafunzi na mali nyinginezo vimekadiliwa kuwa na
thamani ya shilingi milioni 200
Aidha Katibu wa
bodi na ambaye ni mkuu wa shule ya sekondari ya mt Alfred Spriani Vumilia
alisema mara baada ya ya tukio hilo zilipelekwa taarifa wizara ya elimu
na mafunzo ya ufundi uongozi wa wizara umeshauri mabweni hayo kujengwa upya na
kuwekewa miundombinu ya usalama kwa wanafunzi.
“Kwa sasa
tunasubiri kufanya uchambuzi wa vyanzo vya mapato na kutafuta wahisani au
wafadhili wa shule ili kujenga mabweni mapya kama ilivyoshauri wizara ya
elimu na mafunzo ya ufundi”.Alisema Vumilia.
Kwa sasa
wanafunzi wa kiume wa kidato cha pili na tatu waliounguliwa na mabweni
wanasaidiwa na wazazi na wasamalia kupata mavazi na vifaa vya kujifunzia na
wanaishi na wenzao katika mabweni mengine yaliyosalia kwa kulala wanafunzi
wawili katika kitanda kimoja shuleni hapo.
No comments:
Post a Comment