Thursday, June 27, 2013

MIGOGORO YA ARDHI KIKWAZO CHA MAENDELEO KAGERA

Karagwe
Migogoro ya Aridhi iliyokithiri katika wilaya ya Kyerwa na Karagwe imeelezwa kuwa chanzo chake kikubwa ni viongozi wa serikali za vijiji na Vitongoji kugawa ardhi bila kufuata sheria ,kanuni na utaratibu.
Hayo yalibainishwa jana na mkuu wa mkoa wa kagera kanal mstaafu Fabian Inyasi masawe wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari mkoani humo.
 
Kanal Mstaafu Masawe amesema kuwa,viongozi wa serikali ya vijiji na vitongoji wamechangia kuwepo kwa migogoro ya ardhi baina ya wakulima na wafugaji katika wilaya mbalimbali za mkoa huo ikiwemo wilaya ya karagwe na Kyerwa ambapo migogoro hiyo imekithiri sana.
 
Alizitajabaadhi ya  kata zilizokithiri kwa migogoro  hiyo ni pamoja na kata ya Rugu ,Nyakasimbi Rugera na kihanga kuwa kata hizo zinachangiwa na viongozi wa ngazi za chini.
Kauli ya mkuu wa mkoa huyo ilitokana na barua ya malalamiko kwake kutoka kijiji cha Mililo Ruhita kata ya Rugu  ya May 29 mwaka huu iliyodai mwenyekiti wa kitongoji hicho kuwatapeli wananchi hao zaid ya kaya 100 na kuwauzia  ardhi kinyume cha utaratibu  na bila stakabadhi kiasi cha million 50.
 
Kwa mujibu wa malalamiko ya wananchi hao ambao walimtaja mwenyekiti huyo wa kitongoji kuwa ni Tiziwa Mkolelanda,walisema kuwa watanzania wanaoishi kwenye maeneo hayo ,hutengewa ardhi kidogo ambapo eneo kubwa huuziwa wanyarwanda kwa ajili ya malisho.
 
Katika hatua nyingine wananchi wa kata ya Rugera Wilayani humo wamewalalamikia baadhi ya wananchi wapatao 12 ambao wanahusishwa na tuhuma ya kuvamia ardhi ya kijiji na kujigawiya maeneo makubwa  ukiwemo uvamizi wa ardhi unaosababishwa na wamiliki wa Block(vitalu)
 
Kanali Massawe alisema kuwa waliouziwa ardhi kinyume cha utaratibu watangolewa na kamati ya ulinzi na usalama kwa kushirikiana na wananchi.
         “Ardhi ni mali ya Serikali ya kijiji hao watu waliouziwa  mbuzi kwenye gunia na walio husika ni lazima wachukuliwe hatua”Alisema Massawe.
 
Aidha alisema kamati ya ulinzi na usalama haina budi kusuruhisha migogoro hiyo na kuwa watu wa kata ya Rugu watoe ushirikiano wa dhati ili kumaliza migogoro hiyo inayoweza kuhatarisha usalama wa Raia ambapo aliongeza kuwa mipaka ya kata ya Rugera na wilaya ya Muleba watalamu walishatoka  mkoani kusuruhisha matatizo hayo.
Hata hivyo amewataka wananchi wa kata zilizo na migogoro ya ardhi wenyeviti wao wa vitongoji na vijiji wasichaguliwe tena maana wameshiriki kuhatarisha migogoro katika jamii.

No comments:

Post a Comment