Thursday, June 27, 2013

UKITIMIZA WAJIBU NI HALALI KUPEWA HAKI YAKO

Karagwe
 
Serikali mkoani kagera imemtaka mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya karagwe kuwalipa wanamgambo 52 kiasi cha shilingi million 25 walioshiriki kudhibiti magendo ya kahawa  kwenda nje ya nchi na uvunaji wa kahawa mbichi Hayo yalisemwa jana na mkuu wa mkoa wa kagaera kanal mstaafi Fabiani Inyasi masawe wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari mkoani humo.
 
Kanali mstaafu Massawe alisema kuwa madai hayo ni halali ,mkurugenzi mtendaji wa halmashauri hana budi kuwalipa na kuwa kutowalipa wanamgambo hao ni kitendo cha unyanyasaji,udhalilishaji,ambapo aliongeza kuwa wilya ya karagwe na Kyerwa  katika msimu huo walipata zaid ya shilingi 200 kutokana na mauzo ya kahawa,kuwa ahaoni kwa nini wanamgambo hao wasilipwe stahiki yao.
 
Alisema wananchi wa wilya hizo hawana budi kupiga marufuku magendo ya kahawa kwenda nje ya nchi ,kwamba mauzo ya kahawa ndiyo yanasababiswa kuwepo kwa miundo mbinu mizuri ya barabara ,huduma bora ya afya na mashule.
 
Aliongeza kuwa wanamgambo hao kulinda na kudhibiti kahawa ilikuwa ni kwa maslahi ya Taifa na Halmashauri zao  na wananchi wa wilya hizo ,na kuwa ni marufuku kuendeleza vitendo vya magendo ya kahawa  katika mkoa huo  na kuwa atakaye bainika anakahawa na gari vitataifishwa na nipamoja na kufunguliwa mashtaka.
 
Kwa mjibu wa barua ya wanamgambo hao iliyonakirishwa kwa mkuu wa mkoa wa kagera  ya May 11 mwaka huuwalisema kuwa walipewa kazi hiyo na Halmashauri ya wilya ya karagwe April 16 mwaka 2012 na halmashauri imeendelea kukaidi madai yao.
 
Walisema kuwa walifanya kazi  hiyo kwa mda wa siku 195 kwa makubaliano ya kulipwa shilingi 5000 kwa siku,ambapo kila mwanamgambo alipaswa kulipwa kiasi  cha shilingi 975,000 na kuwa hadi sasa walilipwa kiasi cha shilingi 725,000 kwa kila mmoja.
 
Aidha walisema kuwa kwa malipo ya sasa ,wanamgambo hao wanadai  siku 50 kwa kila mmoja zenyetahamani ya shilingi million 25 na kuwa kwa mda mrefu  familia zao zimeishi kwenye mazingira magumu na watoto wao kurudishwa kukosa michango mbalimbali wakati Halmashauri ikitambua deni hilo.
 
Hata hivyo katika barua hiyo waliendeleza kuwa,wamekuwa wakipewa vitisho na baadhi ya viongozi wa Halmashauri na serikali kuwa vinawakatisha tama katika shughuli za utendaji.

No comments:

Post a Comment