Katika
uchaguzi uliofanywa kuhusu unyanyasaji wa kijinsia imebainika kuwa jumla ya
matukio 529 ya unyanyasaji ikiwemo kubakwa kukatwa mapanga na kupewa mimba za
utotoni. Yamelipotiwa polisi katika wilaya ya Kayagwe.
Hayo
yamesemwa na Bi Ashura kajura kwa niaba ya Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri
ya wilaya ya Karagwe katika mkutano wa unyanyasaji wa kijinsia katika jamii
uliofanyika katika ukumbi wa Community Habilant education Management (CHAMA)
uliopo omulushaka Karagwe.
Bi
Kajuna alisema kuwa kwa miaka miwili 2011 na 2012 Jumla ya matukio 529 ya
unyanyasaji kijinsia yakiwemo ya ubakaji 59 kukatwa mapanga 32 na mimba za
utotoni 30 yalilipotiwa polisi katika wilaya hiyo.
Aliendelea
kusema kuwa unyanyasaji ni udhalilishaji anaofanyiwa mtu kutokana na jinsia
yake na kuwa asilimia kubwa wanaonyanyaswa ni wanawake kutokana na uonevu
unaopangwa na kukubaliwa na Mila na desturi.
Kajura
amevitaja vyanzo vya unyanyasaji kuwa ni pamoja na mila na desturi sheria ya
ndoa ya kiislamu kuozwa kwa nguvu ukeketaji wa mtoto wa kike, kunyimwa haki ya
kutoa maoni ya ukosefu wa Elimu kwa watoto wa kike unaowapelekea kutojiamini na
kuwa katiba kuiweka wazi haki za mwanamke.
Kwa
upande wake Aman Ndabatunga ambaye alishiriki katika mdaharo huo alisema kuwa
chimbuko la tatizo la unyanyasaji wa kijinsia katika jamii ni kutokana na mfumo
dume ambao siku zote ulimwona mwanamke kuwa kiumbe Taifa
Ndabatunga
aliendelea kusema kuwa kutokana na unyanyasaji huo kuna athari nyingi
ziliojitokeza katika jamii ambazo amezitaja kuwa maambukizi ya ugonjwa wa
ngono, kuchoka mwili na kuzeeka kutojiamini na kuthaminiwa kutokuwa na maamuzi
kusababisha ulemavu na kifo na kukuwa vifo na kuwa zaidi ya asilimia 50 ya
wanawake walio katika ndoa wanabakwa na waume zao.
Tumeshuhudia
wamanaume wakiwapa watoto wao wa kuzaa na akiamua kumchukuliwa hatua za
kisheria anaambiwa hayo ni masuala ya mila na desturi hupaswi kuwaingilia
ambapo watoto wanazidi kuteseka kutokana na mila na desturi zilizopitwa na
wakati Alisema Ndabatunga.
Naye
sabron kuwa mkwazi wa kitongoji cha mgaba kijiji cha Bujara anayetuhumiwa
kumbebesha Mimba mwanae wa kuzaa mwenye umri wa miaka 15 mwanafunzi wa darasa
la saba baada ya kufikishwa kwenye ofisi ya kijiji hicho aliojiwa kuhusu tuhuma
hizo ambapo alikana kosa hilo.
Kwa
mujibu wa maelezo yaliyotolewa na mtoto ambaye anakabiliwa kuwa na ujauzito wa
miezi sita alisisitiza kuwa baba yake ndiye aliyempa ujauzito huo.
“Tulikuwa
shambani tunapalilia ndipo baba aliponitaka kimapenzi na baada ya kukataa
alinishikia panga na kusema atanua na kutokana na hofu zikuweza kupiga kelele
kwa kuhofia kuwa ataniua na kutokana na hofu sikuweza kupiga kelele kwa kuofia
kuwa ataniua “ Alisema mtoto huyo”
Aliendelea
kusema kuwa baada ya kuwa baada ya kurudi nyumbani hakuna lolote kwa kile alichosema
kuwa aliambiwa endapo angesema chochote angeuwawa na baba yake.
“Niliendelea
kunyamaza japo nilikuwa nahisi maumivu mwili mzima na baba aliendelea
kunifanyia mapenzi mpaka akanipa mimba na nilipojisikia kuwa nina mimba
niliamua kumwambia mama” Alisema mtoto huyo.
Kwa
upande wake mama wa mtoto huyo alipoulizwa kuhusu suala hilo alisema kuwa baada
ya kugundua mwanae kuwa ana ujauzito
alitoa taarifa kwenye ofisi ya kijji ndipo taratibu za kumkamata baba wa mtoto
huyo zilifuata.
Aidha
baada ya kukana tuhuma hizo za kumpa mimba mwanae aliachiwa huru ambapo
wananchi walimfukuza kijijini humo na hatimaye kutokomea kusikojulikana.
Lakini
Owokusima Kaihura kutoka ofisi ya ustawi wa jamii wilayani Karagwe alipoulizwa
kuhusu vitendo hivyo alisema kuwa baadhi ya wazazi hawatoi taarifa za matukio
hayo kutokana na uelewa mdogo walionao na kuwa wengine hukandamizwa na mila na
desturi.
Saulo
Malauri kutoka shirika la Mamas` Hope organization for legal assistance (MHOLA)
alisema kuwa kuafuatia matukio hayo shirika lake aliamua kutoa huduma za
kisheria kuhusu akina mama na watoto ili
kupunguza vitendo hivyo vinavyojitokeza.
Shirika
letu lipo Bukoba na tunatoa Elimu ya Kisheria kuhusu haki za hakina mama na kwa
jinsi matokeo yanavyozidi kupamba moto tumeamua kuweka ofisi zetu kila wilaya
na kutua mfumo ili jamii iweze kuwa na uelewa zaidi kuhusiana na vitendo hivyo
vinavyotishia amani katika jamii yetu Alisema malauri.
Kwa
mujibu wa maelezo yaliyotolewa na mwenyekiti wa asasi ya Karagwe Development
Network of volunteers organization (KADENVO) Bw. Telesphory kalemela chini ya
udhamin mtandao wa kufatilia sera mwanza (Initiative alisema kuwa jamii
inastahili kuelimishwa juu athari za unyanyasaji ikiwa ni pamoja na kuachana na
mila na desturi zilipitwa na waakti ambazo hupelea unyanyasaji huo.
Hata
hivyo washiriki katika mdhaharo huo wametakiwa kutoa elimu katika jamii
inayotuzunguka ili kuondokana na tatizo hilo ikiwezekana kutokomeza kabisa.
No comments:
Post a Comment