Halmashauri
ya wilaya Karagwe mkoani kagera imelalamikiwa kutowajali watu wenye ulemavu wa
ngozi, walemavu wa viungo, watoto yatima wakiwemo wanawake wajane yakiwa ni
makundi yenye malengo yanayofanana.
Hayo
yalisemwa jana na mwenyekiti wa umoja wa wanawake (UWK) katika wilaya ya
karagwe na kyerwa Grace Mahumbuka wakati akifungua mkutano wa mabaraza ya
katiba ya asasi. Taasisi na makundi ya watu wenye malengo yanayofanana.
Mahumbuka
alisema kuwa uongozi wa Halmashauri umekuwa hauwathamini watu walio katika
makundi yanayofanana huku wakiwa dhalilisha pale wanapokuwa wanahitaji msaada
ikiwemo kupewa kejeli na baadhi ya viongozi wa halmashauri.
“Viongozi
wa halmashauri wanatuchukulia kama labda sisi tulipenda tuwe hivi kama tulivyo
umeshuhudia mwenyewe tulivyonyimwa ukumbi na kufukuzwa kama watoto na umeona
tunavyofanyia mkutano kwenye uwanja wa michezo na ukumbi wamepewa wenye pesa”
Alisema mahumbuka.
Alisema
kwa mujibu wa kifungu cha 18(6) cha sheria ya madiliko ya kariba sura ya 83
tume imeweza kuruhusu asasi, taasisi na makundi ya watu wenye malengo
yanayofanana kuandaa mikutano kutoa maoni yao juu ya rasimu ya katiba
Alisema
katika kuziwezesha asasi taasisi na makundi ya watu wenye malengo yanayofanana
kuunda mabaraza ya katiba tume imeruhusu kuendesha mkutano kuipitia barua yenye
Kumb.Na. 76/386/02/150 ya julai 18 mwaka huu.
Alifafania
kuwa tume ya mabadiliko ya kwa mujibu wa sheria ya mabadiliko ya katiba sura ya
83 kifungu cha (22)1 limeweka wazi upatikanaji wa wajumbe 166 kutoka katika
makundi ya watu wenye malengo yanayofanana.
Aidha
katika uchunguzi huo uliofanyika katika uwanja wa michezo wa kayanga wilayani
humo Grace mahumbuka alichaguliwa kuwa
kuwakilisha kundi la wanawake wajane, Agnes Mukuta (Madhehebu), Coletha
Brikmas (Walemavu wa viungo) Savela Aaron wanaishi na virusi vya UKIMWI.
Aliwataja
wengine waliochaguliwa kuwa ni pamoja Generoza katto kundi wakulima vyama vya
siasa Henerico Ernest, Neema Edward (Elimu ya juu na Brasio Stephano watu wenye
ulemavu wa ngozi.
Naye
mwenyekiti wa Halmashauri hiyo walles mashanda alikanusha tuhuma iliyoelekezwa
kwake dhidi ya halmashauri yake kutowajali watu walio kwenye makundi
yanaylofanana.
Mashanda
alisema kuwa hawakuweza kupewa ukumbi kutokana na ukumbi huo kukodishwa kwa
mwezi mmoja kwa asasi nyingine na kuwa umoja wa wanawake walileta maombi yao
kwa kuchelewa.
Hata
hivyo alisema kuwa halmashauri hiyo imekuwa karibu na makundi hayo akiongeza
kuwa wanaykoshule ya watoto wenye ulemavu wa ngozi Kitengule walitoa ofisi ya
walemavu wa viungo katika majengo yao na kuwa wamekuwa wakishirikiana na ofisi
ya umoja wanawake kwa kila jambo.
No comments:
Post a Comment