Monday, January 18, 2016

ASHIKILIWA NA JESHI LA POLISI KWA TUHUMA ZA KUMUUA MKE WAKE KWA KIPIGO.





Jeshi la polisi wilayani Missenyi Mkoani Kagera  linamshikilia mtu mmoja kwa kosa la kumpiga na kumuua mke wake.

Tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia Januari11 mwaka huu ,ambapo mwanaume aliyefahamika kwa jina la  Kamala Kamugisha  wa umri miaka 33  mkazi wa kitongoji Bwoba kijiji cha Kashaba wilayani Missenyi amemuua mkewe kwa kumpiga sehemu mbalimbali za mwili wake.

Akizungumzia tukio hilo Baba Mkwe wa maraehemu Mzee Karoli  Kamugisha  amesema kuwa kijana wake ambaye ni mtuhumiwa sasa,amekuwa na ugomvi wa siku nyingi na mkewe hali ambayo imepelekea hadi kifo hicho.

Mzee Karoli amesema kuwa marehemu  Laulensia Kamala usiku alikimbilia kwa baba mkwe akidai  kupigwa na mmewe,ambapo alfajiri amekata roho wakiwa kwenye harakati za kumkimbiza hospitalini.

Afisa mtendaji Abdalah  Lutaiwa wa kijiji Kashaba amesema kuwa marehemu ameuwawa kwa kupigwa mateke na ngumi sehemu mbalimbali za mwili wake,huku akiwaasa wanaume ambao ni vijana kuacha tabia ya kujichukulia sheria mikononi kwa kuwadhuru wake zao.

Amesema ili kukomesha vitendo hivyo watahakikisha wanawachukulia hatua kali za kisheria wanaume ambao watakuwa wanajihusisha na vitendo vya kuwanyanyasa wanawake katika familia.

Hata hivyo jeshi la polisi  wilayani humo limeruhusu mwili wa marehemu kuzikwa na mtuhumiwa  anashikiliwa kwa ajili ya hatua zaidi za  uchunguzi.

No comments:

Post a Comment