Saturday, January 2, 2016

FAMILIA YA RAIS YATAPELIWA HUKO HANDENI MKOANI TANGA BAADA YA KULIPIA ARDHI FEKI.




Familia  ya  aliyekuwa   Rais  wa  tano  wa  Zanzibar  DK Salmin   Amour  imetapeliwa  katika  kijiji  cha  Magamba   kata  ya  Kwaluguru   wilayani  Handeni   mkoani  Tanga  kwa  kuuziwa  ekari  150  za  ardhi   kwa  ajili  ya  shughuli  za  kilimo   na  baadae  kubainika  kuwa  eneo  hilo  lilitengwa   kwa  ajili  ya  hifadhi  ya  kijiji  hicho.


Afisa  mtendaji  wa  kijiji  cha  Magamba Erick  Semsela  alikiri  kupokea  kiasi  cha  shilingi   millioni  mbili  kwa  ajili  ya  kuuza  eneo  hilo  la  hekari  50  tu na  siyo  eneo  lote  la  hekari  150  kama  inavyodaiwa  huku  akibainisha  kuwa  eneo  la  hifadhi  ni  hekari  15  tu.
 

Diwani  wa  Kata  ya  Kwaluguru  Salimu Muya  ameunda  kamati  itakayochunguza  migogoro  ya  ardhi  katani  humo  na  kuipa  siku  14  na  baadae  watoe  majibu  ya  uchunguzi  huo   na  kusema  kuwa  fedha  na  stakabadhi  za  hekari  100  hazionekani  mahali  ziliporekodiwa  wakati   mnunuzi  anadai  alilipa  pesa  yote  na  adaiwi.

Mwakilishi  wa  familia  ya Rais  Mstaafu  Munil  Amour  amesema  mwaka  2015 walifika  kijijini  hapo wakitafuta eneo  la  kufanyia  shughuli  za  kilimo  na  kupatiwa  eneo  hilo  na  kufanya  malipo  lakini  baadae  ndipo  ikabainika  kuwa  ni  eneo  la  hifadhi  na  hawajui  lini  watapatiwa  majibu  ya  ufumbuzi  wa tatizo  hilo.

No comments:

Post a Comment