Saturday, January 2, 2016

MKOA WA MOROGORO WA UANZA MWAKA 2016 KWA AJALI ZAUA WATU SITA NA 25 WAJERUHIWA .


 Watu  sita  wamefariki  dunia  na  25 kujeruhiwa   katika  ajali  mbili   tofauti  zilizotokea  eneo  la Iyovi katika  daraja mto  Ruaha   na  Dumila  mkoani  Morogoro




 Kamanda  wa  polisi  mkoa  wa  MOROGORO  Leonald  Paulo  amesema   tukio  la  kwanza  lilitokea  eneo  la  Msosa  mpakani    mwa  Morogoro   na  Iringa   katika  daraja  la   Mto  Ruaha katika  mto   mdogo  wa  Mkosi  ambapo  watu  watatu  walifariki  dunia    na  wengine  20  kujeruhiwa  vibaya.













Katika  ajali  ya  pili  iliyotokea  leo  Januari  02  mwaka  huu  2016   majira  ya  asubuhi  eneo  la  Dumila   watu   watatu  wamefariki   dunia  papo  hapo  baada  ya  gari   ndogo  aina  ya   Toyota  Vista  kugongana  uso  kwa  uso   na  lori  lililokuwa  na   tela  lake   na  kwenye  ajali  hiyo  watu  watano  wamejeruhiwa.

No comments:

Post a Comment