Monday, January 11, 2016

FAMILIA YA WATU 8 WANUSURIKA KIFO BAADA YA KURA CHAKULA KILICHOWEKEWA SUMU NA WATU WASIOJULIKANA USIKU.




Watu wanne wa familia moja katika kijiji cha Nyakahita kata ya kanoni wilayani karagwe wamenusurika kufa baada kutegewa sumu kwenye chakula usiku wa kuamkia leo januari 11 mwaka huu.


Familia hiyo yenye jumla ya watu wa nane wamewekewa sumu katika chakula na  wengine wanne walinusurika kura chakula hicho baada ya kuwaona wenzao walioanza kura chakula hicho wakisumbuliwa na tumbo.


Akizungumzia juu ya tukio hilo Mwenyekiti wa kijiji hicho ambaye pia ni shuhuda ya tukio hilo CHRISTOPHER JUSTINIAN ameeleza kuwa baada ya tukio hilo walitakiwa kuitisha kikao cha dhalura cha kijiji na kuwataka wananchi kutochukua maamuzi magumu yanayo gharimu maisha ya watu wengine katika jamii wanapokwazwa na ndugu, jamaa na rafiki.


Aidha mwenyekiti huyo ameongeza kuwa watu wanatakiwa kumjua mungu kwa kufanya maombi ili kuepusha matatizo yanayo endelea kutokea katika jamii na endapo mwenzako akakukosea ni vyema ukampeleka katika vyombo vya sheria kuliko kujichukuria sheria mkononi.

No comments:

Post a Comment