Katibu Tawala
wa Mkoa wa Kagera
Nassoro Mnambira amemvua
madaraka Mkuu wa
Shule ya Sekondari
Bilele iliyoko Manispaa
ya Bukoba Siasa
Phocus kwa kukiuka
maelekezo ya serikali
kwa kuwataka wazazi
na walezi wa wanafunzi
kutoa fedha ya michango
ikiwemo shilingi elfu
arobaini za uji
na fedha za
mlinzi shilingi elfu
tano.
Amesema kitendo cha
mkuu huyo kutoza
michango hiyo ni
kukiuka agizo la
Rais aliyesema elimu
ni bure huku
akitoa ufafanuzi juu
ya mkoa wa
Kagera kupokea fedha
kutoka hazina kwa
ajili ya kutekeleza
tamko la elimu bure.
Kupitia wizara ya elimu
na mafunzo ya ufundi mkoa wa KAGERA umepokea shilingi milioni 810 laki moja na
57 elfu kwa awamu ya kwanza ili kutekereza sera ya elimu bure.
Akizungumza na waandishi
wa habari katibu tawala wa mkoa wa KAGERA NASORO MNAMBIRA amesema kuwa milioni
309 laki nne 61 elfu zimepelekwa katika shule za msingi huku zaidi ya milioni
mia tano zikipelekwa katika shule za sekondari mkoani KAGERA.
Akitoa ufafanuzi
wa fedha hizo zilivyopokelewa katika halmashauri za mkoa wa KAGERA amesema kuwa
kwa upande wa shule za sekondari wilaya ya Bihalamuro imepokea milioni
76,halmashauri ya Bukoba ya milioni 36 Bukoba manispaa milioni 122 Karagwe milioni
36 Kyerwa milioni 21 Missenyi milioni 29 muleba shilingi milioni 93 na Ngara shilingi milioni 60.
Kwa upande wa fedha
zilizopokelewa katika shule za msingi kwa mkoa wa KAGERA wilaya ya Buhalamuro
imepokea shilingi milioni 43,halmashauri ya Bukoba zaidi ya milioni 36, bukoba
manispaa zaidi ya milioni 27 karagwe zaidi ya milioni 37 kyerwa zaidi ya milioni
37 misenyi zaidi milioni 20 Muleba milioni 69 na Ngara milioni 37.
No comments:
Post a Comment