Tuesday, January 19, 2016

KESI YA KUPINGA MATOKE YA UBUNGE JIMBO LA KYERWA KUANZA KUSIKILIZWA JANUARI 21 MWAKA HUU.






Kesi ya kupinga matokeo ya Ubunge ya uchaguzi mkuu 2015  jimbo la Kyerwa Mkoani Kagera inatarajiwa kuanza kusikilizwa kwa mara ya kwanza Alhamisi ya tarehe 21 januari mwaka huu.


Akiongea na MTANDAO HUU aliyekuwa mgombea wa ubunge katika jimbo hilo kupitia Chama cha Demokrasia na maendeleo CHADEMA, Benedicto Mtungirehi amesema baada ya kufuata taratibu za mahakama zilizokuwa zinahitajika sasa kesi hiyo inategemewa kusikilizwa kwa mara ya kwanza.

Mtungirehi amesema amekuwa akipokea maswali mengi kutoka kwa wananchi wa Jimbo la Kyerwa kuhusu  kesi iliyofunguliwa Mahakama Kuu Kanda ya Bukoba ambapo amesema kuwa ilikuwa vigumu kuwajibu kwani kesi ilikuwa bado  haijaanza kusikilizwa lakini sasa kesi hiyo itasikilizwa kwa mara ya kwanza januari 21 mwaka huu.


Ameeleza kuwa siku ya Alhamis mshitaki na mshtakiwa wanatakiwa kufika katika mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Bukoba kwa ajili ya kupanga mambo ya msingi ya namna ya kuendesha kesi hiyo.

No comments:

Post a Comment