Thursday, January 14, 2016

SERIKALI YA AWAMU HII UKIPATA NAFASI TOA MAAGIZO WA MUDA MAALUMU MKUU WA MKOA ASEMA WATOTO WOTE WAWE DARASANI KUFIKIA MACHI MOSI MWAKA HUU


 
Mkuu wa mkoa wa Kagera John Mongella amewataka  wazazi,walezi na Jamii kwa ujumla kuwapeleka watoto wote wanaotakiwa kujiunga na elimu ya msingi pamoja na sekondari mapema iwezekanavyo kabla ya kuchukuliwa hatua za kisheria.






 
Ameyasema hayo mapema leo  katika ziara yake ya kukagua usajili wa wanafunzi unavyoendelea katika wilaya  ya Karagwe.


Hata hivyo ametembelea mradi wa ujenzi wa chuo cha ualimu uliopo Kata ya Ihanda wilayani hapa na kuhaidi kutoa ushilikiano juu kumalizia mradi huo.


Aidha  ametoa  agizo  kwa  uongozi  wa  wilaya  ya  Karagwe kuhakikisha  ifikapo  Machi  Mosi  mwaka  huu  watoto  wote  wawe wameisharipoti    madarasani  kwani  ni lengo  la  mkoa  mzima  wa  Kagera  kwa  tarehe  hiyo.

No comments:

Post a Comment