Hatima ya
maombi ya wakazi
wa jimbo la
Kinondoni ambao nyumba zao
ziko katika orodha
ya bomoabomoa itajulikana kesho
mahakama ya kuu
kitengo cha Ardhi
itakapotoa uamuzi wa maombi
yao ya kusimamisha
uamuzi wa serikali kuwabomolea ili kusubiri usikilizwaji wa maombi
yao ya kibali cha
kufungua kesi kupinga
ubomoaji huo.
Wakili wa wakazi
wa Kinondoni ,Abubakar Salum aliiomba Mahakama itoe
amri kwamba hali iendelee
kuwa kama ilivyo kwa
sasa kusubiri usikilizwaji
na uamuzi wa maombi
ya kibali cha
kufungua kesi lakini wakili
wa serikali Gabriel
Malata alipinga ombi hilo akidai kuwa waombaji hao
hawana haki ya kuomba
amri yoyote ya mahakama
katika hatua hiyo
ambapo Mahakama haijawapa
kibali cha kufungua
kesi.
Jaji
Panterine Kente baada
ya kusikiliza hoja za pande zote
alisema kuwa atatoa uamuzi
wake kesho saa tano iwapo hali ilivyo kwa sasa iendelee au la.
No comments:
Post a Comment