|
|
Takwimu Na hali ya
Ukimwi Tanzania
Siku ya Ukimwi dunian
ilianzishwa maalumu kuadhimishwa siku ya
tarehe 1.12. kila mwaka kwa kuwa siku ya kwanza
kugundua kirus kinachoeneza ugonjwa
wa Ukimwi kiligunduliwa siku ya tarehe 1.12 .mwaka 1981
Mwaka 1983 ndo
mgonjwa wa kwanza wa Ukimwi aligunduliwa
katika hospitali ya Ndolage iliyopo mkoani Kagera
mgonjwa huyo alitokea kijiji cha Kanyigo Bukoba vijijini sasa wilaya ya
Missenyi.
Tangu kugunduliwa kwa ugonjwa
wa Ukimwi nchini mwetu watu wapatao 1.3 milion wanaishi na virusi vinavyoeneza
ugonjwa wa Ukimwi na kati ya hao watu wapatao 384,816
tayari wameanzishiwa dozi ya dawa
ya kupumbaza virus vya Ukimwi yaani ARV’S
na watu wapatao 86,000 wamepoteza maisha kutokana na ugonjwa
wa ukimwi na kuacha watoto yatima
2 milion kutokana na kufiwa na wazazi wao na kupoteza nguvu kazi ya
Taifa.Kuanzia Julai 2007 watu 13 milion wapima afya zao kwa hiari
na Ushauri Nasaha pale rais wa JAKAYA
KIKWETE alipozindua kampein ya
upimaji wa hiari imesaidia kupunguza unyanyapaa.
Kufikia Desembar 2010
watu wapatao 740,040
wanaoishi na virus vya
Ukimwi walipata huduma ya matibabu na uangalizi,na kati ya hao
384,816 wako katika dozi ya ARV’S hii ni
sawa na 87.5 ya walengwa kupata matibabu.Kwa sasa kuna vituo 4,301 vya kutoa huduma ya kinga ya
maambukizi ya mama kwenda mtoto(PMTCT) Ikiwa ni sawa na 93% kwa vituo
vya afya vilivyolengwa.Kufikia mwaka 2010 wanawake wajawazito waliokuwa
wakiishi na HIV ni 80,748 sawa na 70% na
kati ya hao 65,948 waliopata matibabu sawa na 57% na walipokea madawa ya
kukinga maambukizi ya HIV kutoka kwa
mama kwenda kwa mtoto.
Kwa Takwimu
zilizotolewa na Tume ya Kudhibiti
Ukimwi Tanzania TACAIDS kuhusu hali ya maambukizi Tanzania Kwa mujibu wa utafiti uliofanywa mwaka
2007-2008 kiwango cha maambukizi kitaifa
kilishuka kutoka asilimia 7.7 ya mwaka 2003-2004 mpaka 5.1 huku mikoa 5 inayoongoza kwa mujibu wa
takwimu za mwaka 2007/2008 ikiwa ni
Iringa 15.1%,Dar-es salaam 9.3%, Mbeya
9.2%,Mara 7.7% na Shinyanga 7.4%
huku mkoa unaoongoza kwa maambukizi mpya hivi sasa ni Mara ambao umeongeza 3.5% kutoka 4.2% za mwaka 2003/2004 nakufikia 7.7%
za mwaka 200/2008.
Wilaya zinazoongoza
kwa maambukizi kitaifa kwa sasa
ni Makete ya mkoa wa Iringa ,Rory kwa Mkoa wa Mara .
|
Kwa
Ujumla neno mtando lina maana ya mfumo au kikundi chochote kilichounganishwa.
Hii ni njia mojawapo ya kubadilishana habari kati ya mifumo tofauti. TACAIDS
inaratibu mitandao mbalimbali ya mapambano dhidi ya UKIMWI. Ifuatayo ni
baadhi ya miandao hiyo:
- NETWO+: Ni Mtandao wa Taifa
wa Wanawake wenye VVU/UKIMWI
- ICW: Ni Jumuiya ya Kimataifa
ya Wanawake wanaoishi na VVU/UKIMWI
- MNEYOP+ : Ni Mtandao wa Taifa
wa Vijana wenye VVU/UKIMWI
- TANGYWA+:Ni Mtandao wa Taifa
wa Wasichana na Wanawake Vijana wanaoishi na VVU/UKIMWI Tanzania
- TANEPHA:Ni mtandao wa Asasi
za Watu wanaoishi na VVU/UKIMWI Tanzania
- TANERELA :Mtandao wa Viongozi
wa Dini wanaoishi au walioathiriwa na VVU/UKIMWI Tanzania
- NYP+ :Mtandao wa Vijana
wanaoishi na VVU/UKIMWI
- NACONGO :Baraza la Taifa la
Asasi zisizo za Serikali
- TAYOPA :Balozi wa Vijana
wanaoishi na VVU/UKIMWI Tanzaniaa
- FONEPHAT :Mtandao wa Kitaifa
wa watu wanaoishi na VVU/UKIMWI
- NACOPHA:Baraza la Taifa la
watu wanaoishi na VVU/UKIMWI Tanzania
NACOPHA: Ni Baraza la Taifa la Watu wanaoishi na VVU/UKIMWI Tanzania
ni asasi isiyo ya serikali iliyoanzishwa mwaka 2003 kwa madhumuni yaliyotajwa
katika kifungu cha 2.4 cha katiba yao kama ifuatavyo: Kuwakutanisha watu
wanaoishi na VVU/UKIMWI kwa madhumuni ya kuongeza ushiriki na kuongeza uwezo
wao wa kushawishi katika majukumu yao katika kufanikisha mapambano dhidi ya
VVU/UKIMWI nchini Tanzania. NACOPHA ilianzishwa kama asasi mwavuli kwa mujibu
wa dira na dhamira iliyotajwa katika katiba yao.
FONEPHAT: Ni Mtandao wa Kitaifa wa watu wanaoishi na VVU/UKIMWI. Ni
asasi mwavuli kwa ajili ya mitandao, vikundi na vyama vya watu wanaoishi na
VVU/UKIMWI nchini. Ina jukumu la kuratibu mitandao ya WAVIU Tanzania.
FONEPHAT ilianzishwa mwaka 20 Oktoba, 2007 mjini Dar es Salaam ambapo kwa
sasa inaratibu mitandao 12 ya kitaifa ya WAVIU. FONEPHAT ina bodi na
sekretariati.
TAYOPA: Ni Balozi wa Vijana wanaoishi na VVU/UKIMWI Tanzania.
Ilianzishwa mwaka 1998 na kusajiliwa rasmi mwaka 2001. Inaongozwa na
Mwenyekiti, Katibu na Mweka Hazina. Vile vile ina kamati ya utendaji, maamuzi
makuu hufanywa na mkutano mkuu ambao hukutana kila baada ya miaka mitano (5).
TAYOPA ina matawi 4 katika mikoa ya Morogoro, Mbeya, Ruvuma na Rukwa. Jukumu
kubwa la TAYOPA ni kuelimisha vijana walioko mashuleni na wasio kuwa
mashuleni.
NACONGO: Ni chombo chenye jukumu la kuratibu na kujiratibu kwa asasi
zisizo za serikali zinazofanya kazi Tanzania. NACONGO ilianzishwa kwa sheria
ya Bunge namba 24 ya mwaka 2002, na kuzinduliwa rasmi mwaka 2003.
ICW: Ni Jumuiya ya Kimataifa ya Wanawake wanaoishi na VVU/UKIMWI. Ni
mtandao wa kimataifa pekee unaoendeshwa kwa ajili ya na wanawake wenye
VVU/UKIMWI. Ilianzishwa mwaka 1992 na wanawake 56 wenye VVU/UKIMWI duniani.
Uanachama wa ICW ni huru na unawahusu wanawake wenye VVU/UKIMWI tu. ICU
inahusu masuala na mahitaji yanayowakabili wanawake wanaoishi na VVU/UKIWM
duniani kote na kuunda msingi wa philosophia ya asasi hiyo. Wanawake
walikubaliana wasikate tama na ndio maana walianzisha jumuiya hiyo. ICW
inajihusisha zaidi na uraghbishi kuhusu masuala ya wanawake.
NETWO+: Ni mtandao wa Taifa wa Wanawake wenye VVU/UKIMWI. Mtandao huu
unafanya shughuli zake nchi nzima na unaendeshwa na wanawake wanaoishi
na VVU/UKIMWI. Ulianzishwa mkoa wa Morogoro Decemba 28, 2002 na
kusajiliwa rasmi Mei 30, 2003 kwa namba ya usajili SO11944. Ilianzishwa kwa
madhumuni ya kuunganisha wanawake wanaoishi na VVU/UKIMWI na watu binafsi,
vikundi na asasi zinazosaidia wanawake wenye mahitaji yanayohusiana na
VVU/UKIMWI.
Lengo kuu la mtando huu ni kuongeza fursa ya wanawake wanaoishi na VVU/UKIMWI
za kusikika na kushiriki katika shughuli za kidemokrasia zinazowezesha
kusikika kwa haki zao na serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, wadau
na wahisani wengine.
TANERELA
TANERELA ni Mtandao wa Viongozi wa Dini Waishio na VVU au Walioathiriwa
Binafsi na VVU/UKIMWI. Mtandao huu ulianzishwa kwa nia ya kuwawezesha
viongozi wa Dini wanaoishi na VVU na wale walioathiriwa binafsi kufanya
yafuatayo:
- Kuvunja ukimya na kuwa wazi
kuhusu hali zao;
- kuondoa unyanyapaa binafsi –
Kujinyanyapaa
- kuondoa mtazamo hasi wa
kukana na kukataa ukweli wa hali halisi
- Kuondoa mawazo ya kudhani
kwamba kuwa na VVU ni jambo la aibu
- kuwa chachu ya mabadiliko
kiimani kwa wao wenyewe, kwa Jamii zinazowazunguka na kwa Taifa kwa
jumla
- Makao Makuu ya TANERELA yako
Dar es Salaam lakini pia ina matawi katika mikoa ya Dodoma, Kagera,
Kigoma na Morogoro.
TANOPHA
TANOPHA ni mtandao wa Asasi za Watu Waishio na VVU/UKIMWI ambao ulianzishwa
mwaka 2001 na kusajiliwa 2002. TANOPHA ilianza na asasi wanachama 22 na kwa
sasa ina jumla ya wanachama 110 kwa nchi nzima.
TANOPHA Ilianzishwa kwa lengo la kuzipa nguvu na sauti na kuzisaidia asasi
zinazoendeshwa na kungozwa na watu waishio na VVU katika Tanzania. Makao
makuu ya TANOPHA yako Dar es Salaam
TANEPHA
TANEPHA ni mtandao wa watu waishio na VVU uliosajiliwa mwaka 2003 kwa lengo
la kushirikiana na mitandao mingine ya ndani na nje ya nchi ili kuunganisha
juhudi katika mapambano dhidi ya UKIMWI na kuwa kituo cha Taarifa za
kimataifa kwa WAVIU. Aidha TANEPHA inahusika pia na kufuatilia suala la
upatikanaji wa dawa za kupunguza makali ya VVU kwa walengwa.
TANGYWA+
TANGYWA+ ni mtandao wa wasichana na Wanawake vijana wanaoishi na VVU
ulioanzishwa mwaka 2004 na kusajiliwa mwaka 2007. Mtandao huu unalenga
kudhibiti maambukizo mapya ya VVU, kupigania haki za binadamu, afya ya uzazi
kwa wasichana na wanawake wa umri Mdogo.
Miongoni mwa shughuli za TANGYWA+ ni kuboresha hali za maisha ya wasichana
kwa kutoa huduma zifuatazo:
- Misaada wa kimaadili, na
kisaikolojia kwa wateja wake;
- Misaada ya lishe na vifaa vya
shule kwa watoto yatima;
- kutoa maelekezo na ushauri
kuhusu masuala ya tiba na matunzo kwa wagonjwa wa UKIMWI;
- Huduma za tiba, ushauri na
matunzo nyumbani;
- mafunzo ya stadi za maisha
kwa wasichana
- Hivi sasa mtandao huu
unafanya kazi katika mikoa 8 ifuatayo katika Tanzania Bara: Arusha, Dar
es Salaam, Dodoma, Kilimanjaro,Morogoro, Mwanza, Singida na Pwani.
NNEYOP+
NNEYOP ni mtandao wa kitaifa wa Vijana Wanaoishi na VVU ulioanzishwa na
kusajiliwa mwaka 2006 kwa ajili ya kuchangia juhudi za serikali za kudhibiti
maambukizo ya VVU na UKIMWI nchini Tanzania.
Lengo la NNEYOP+ ni Kuunganisha vijana wanaoishi na VVU waweze kupigania haki
zao na kutetea haki za vijana wanaoishi na VVU yakiwemo masuala ya unyanyapaa
na ubaguzi. Aidha NNEYOP inatetea uimarishaji wa huduma za tiba, matunzo na
misaada kwa vijana waishio na VVU na ushirikishwaji wao kwenye vyombo vya
maamuzi.
Prepared by
Juhudi felix
2012
|
|
Kwa
Ujumla neno mtando lina maana ya mfumo au kikundi chochote kilichounganishwa.
Hii ni njia mojawapo ya kubadilishana habari kati ya mifumo tofauti. TACAIDS
inaratibu mitandao mbalimbali ya mapambano dhidi ya UKIMWI. Ifuatayo ni
baadhi ya miandao hiyo:
- NETWO+: Ni Mtandao wa Taifa
wa Wanawake wenye VVU/UKIMWI
- ICW: Ni Jumuiya ya Kimataifa
ya Wanawake wanaoishi na VVU/UKIMWI
- MNEYOP+ : Ni Mtandao wa Taifa
wa Vijana wenye VVU/UKIMWI
- TANGYWA+:Ni Mtandao wa Taifa
wa Wasichana na Wanawake Vijana wanaoishi na VVU/UKIMWI Tanzania
- TANEPHA:Ni mtandao wa Asasi
za Watu wanaoishi na VVU/UKIMWI Tanzania
- TANERELA :Mtandao wa Viongozi
wa Dini wanaoishi au walioathiriwa na VVU/UKIMWI Tanzania
- NYP+ :Mtandao wa Vijana
wanaoishi na VVU/UKIMWI
- NACONGO :Baraza la Taifa la
Asasi zisizo za Serikali
- TAYOPA :Balozi wa Vijana
wanaoishi na VVU/UKIMWI Tanzaniaa
- FONEPHAT :Mtandao wa Kitaifa
wa watu wanaoishi na VVU/UKIMWI
- NACOPHA:Baraza la Taifa la
watu wanaoishi na VVU/UKIMWI Tanzania
NACOPHA: Ni Baraza la Taifa la Watu wanaoishi na VVU/UKIMWI Tanzania
ni asasi isiyo ya serikali iliyoanzishwa mwaka 2003 kwa madhumuni yaliyotajwa
katika kifungu cha 2.4 cha katiba yao kama ifuatavyo: Kuwakutanisha watu
wanaoishi na VVU/UKIMWI kwa madhumuni ya kuongeza ushiriki na kuongeza uwezo
wao wa kushawishi katika majukumu yao katika kufanikisha mapambano dhidi ya
VVU/UKIMWI nchini Tanzania. NACOPHA ilianzishwa kama asasi mwavuli kwa mujibu
wa dira na dhamira iliyotajwa katika katiba yao.
FONEPHAT: Ni Mtandao wa Kitaifa wa watu wanaoishi na VVU/UKIMWI. Ni
asasi mwavuli kwa ajili ya mitandao, vikundi na vyama vya watu wanaoishi na
VVU/UKIMWI nchini. Ina jukumu la kuratibu mitandao ya WAVIU Tanzania.
FONEPHAT ilianzishwa mwaka 20 Oktoba, 2007 mjini Dar es Salaam ambapo kwa
sasa inaratibu mitandao 12 ya kitaifa ya WAVIU. FONEPHAT ina bodi na
sekretariati.
TAYOPA: Ni Balozi wa Vijana wanaoishi na VVU/UKIMWI Tanzania.
Ilianzishwa mwaka 1998 na kusajiliwa rasmi mwaka 2001. Inaongozwa na
Mwenyekiti, Katibu na Mweka Hazina. Vile vile ina kamati ya utendaji, maamuzi
makuu hufanywa na mkutano mkuu ambao hukutana kila baada ya miaka mitano (5).
TAYOPA ina matawi 4 katika mikoa ya Morogoro, Mbeya, Ruvuma na Rukwa. Jukumu
kubwa la TAYOPA ni kuelimisha vijana walioko mashuleni na wasio kuwa
mashuleni.
NACONGO: Ni chombo chenye jukumu la kuratibu na kujiratibu kwa asasi
zisizo za serikali zinazofanya kazi Tanzania. NACONGO ilianzishwa kwa sheria
ya Bunge namba 24 ya mwaka 2002, na kuzinduliwa rasmi mwaka 2003.
ICW: Ni Jumuiya ya Kimataifa ya Wanawake wanaoishi na VVU/UKIMWI. Ni
mtandao wa kimataifa pekee unaoendeshwa kwa ajili ya na wanawake wenye
VVU/UKIMWI. Ilianzishwa mwaka 1992 na wanawake 56 wenye VVU/UKIMWI duniani.
Uanachama wa ICW ni huru na unawahusu wanawake wenye VVU/UKIMWI tu. ICU
inahusu masuala na mahitaji yanayowakabili wanawake wanaoishi na VVU/UKIWM
duniani kote na kuunda msingi wa philosophia ya asasi hiyo. Wanawake
walikubaliana wasikate tama na ndio maana walianzisha jumuiya hiyo. ICW
inajihusisha zaidi na uraghbishi kuhusu masuala ya wanawake.
NETWO+: Ni mtandao wa Taifa wa Wanawake wenye VVU/UKIMWI. Mtandao huu
unafanya shughuli zake nchi nzima na unaendeshwa na wanawake wanaoishi
na VVU/UKIMWI. Ulianzishwa mkoa wa Morogoro Decemba 28, 2002 na
kusajiliwa rasmi Mei 30, 2003 kwa namba ya usajili SO11944. Ilianzishwa kwa
madhumuni ya kuunganisha wanawake wanaoishi na VVU/UKIMWI na watu binafsi,
vikundi na asasi zinazosaidia wanawake wenye mahitaji yanayohusiana na
VVU/UKIMWI.
Lengo kuu la mtando huu ni kuongeza fursa ya wanawake wanaoishi na VVU/UKIMWI
za kusikika na kushiriki katika shughuli za kidemokrasia zinazowezesha
kusikika kwa haki zao na serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, wadau
na wahisani wengine.
TANERELA
TANERELA ni Mtandao wa Viongozi wa Dini Waishio na VVU au Walioathiriwa
Binafsi na VVU/UKIMWI. Mtandao huu ulianzishwa kwa nia ya kuwawezesha
viongozi wa Dini wanaoishi na VVU na wale walioathiriwa binafsi kufanya
yafuatayo:
- Kuvunja ukimya na kuwa wazi
kuhusu hali zao;
- kuondoa unyanyapaa binafsi –
Kujinyanyapaa
- kuondoa mtazamo hasi wa
kukana na kukataa ukweli wa hali halisi
- Kuondoa mawazo ya kudhani
kwamba kuwa na VVU ni jambo la aibu
- kuwa chachu ya mabadiliko
kiimani kwa wao wenyewe, kwa Jamii zinazowazunguka na kwa Taifa kwa
jumla
- Makao Makuu ya TANERELA yako
Dar es Salaam lakini pia ina matawi katika mikoa ya Dodoma, Kagera,
Kigoma na Morogoro.
TANOPHA
TANOPHA ni mtandao wa Asasi za Watu Waishio na VVU/UKIMWI ambao ulianzishwa
mwaka 2001 na kusajiliwa 2002. TANOPHA ilianza na asasi wanachama 22 na kwa
sasa ina jumla ya wanachama 110 kwa nchi nzima.
TANOPHA Ilianzishwa kwa lengo la kuzipa nguvu na sauti na kuzisaidia asasi
zinazoendeshwa na kungozwa na watu waishio na VVU katika Tanzania. Makao
makuu ya TANOPHA yako Dar es Salaam
TANEPHA
TANEPHA ni mtandao wa watu waishio na VVU uliosajiliwa mwaka 2003 kwa lengo
la kushirikiana na mitandao mingine ya ndani na nje ya nchi ili kuunganisha
juhudi katika mapambano dhidi ya UKIMWI na kuwa kituo cha Taarifa za
kimataifa kwa WAVIU. Aidha TANEPHA inahusika pia na kufuatilia suala la
upatikanaji wa dawa za kupunguza makali ya VVU kwa walengwa.
TANGYWA+
TANGYWA+ ni mtandao wa wasichana na Wanawake vijana wanaoishi na VVU
ulioanzishwa mwaka 2004 na kusajiliwa mwaka 2007. Mtandao huu unalenga
kudhibiti maambukizo mapya ya VVU, kupigania haki za binadamu, afya ya uzazi
kwa wasichana na wanawake wa umri Mdogo.
Miongoni mwa shughuli za TANGYWA+ ni kuboresha hali za maisha ya wasichana
kwa kutoa huduma zifuatazo:
- Misaada wa kimaadili, na
kisaikolojia kwa wateja wake;
- Misaada ya lishe na vifaa vya
shule kwa watoto yatima;
- kutoa maelekezo na ushauri
kuhusu masuala ya tiba na matunzo kwa wagonjwa wa UKIMWI;
- Huduma za tiba, ushauri na
matunzo nyumbani;
- mafunzo ya stadi za maisha
kwa wasichana
- Hivi sasa mtandao huu
unafanya kazi katika mikoa 8 ifuatayo katika Tanzania Bara: Arusha, Dar
es Salaam, Dodoma, Kilimanjaro,Morogoro, Mwanza, Singida na Pwani.
NNEYOP+
NNEYOP ni mtandao wa kitaifa wa Vijana Wanaoishi na VVU ulioanzishwa na
kusajiliwa mwaka 2006 kwa ajili ya kuchangia juhudi za serikali za kudhibiti
maambukizo ya VVU na UKIMWI nchini Tanzania.
Lengo la NNEYOP+ ni Kuunganisha vijana wanaoishi na VVU waweze kupigania haki
zao na kutetea haki za vijana wanaoishi na VVU yakiwemo masuala ya unyanyapaa
na ubaguzi. Aidha NNEYOP inatetea uimarishaji wa huduma za tiba, matunzo na
misaada kwa vijana waishio na VVU na ushirikishwaji wao kwenye vyombo vya
maamuzi.
Prepared by
Juhudi felix
2012
|
No comments:
Post a Comment