Thursday, April 12, 2012

NINAJARIBU KUUTANGAZIA UMMA WATAFUTA KAZI HASWA VIJANA

JAMUHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
OFISI YA WAZIRI MKUU
TAWALA ZA MKOA NA SERIKALI ZA MITAA
HALMASHAURI YA WILAYA YA KILOLO

 TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilolo anawatangazia Watanzia wenye sifa za kujaza  nafasi za kazi  zilizo wazi kama zifuatazo:

NAKAZISIFA ZA MWOMBAJI MAJUKUMUNGAZI YA MSHAHARA NA MSHAHARA
1AFISA MTENDAJI WA KATA DARAJA LA  III (NAFASI (8)
  • Awe amehitimu kidato cha nne au sita.
  • Awe amehudhuria mafunzo ya stashahada ya aina yoyote na kufaulu
  • Awe tayari kufanya kazi sehemu yoyote atakayopangiwa.
  • Awe hajawahi kushitakiwa na kupatikana na  makosa ya jinai
  • Atakuwa Mtendaji Mkuu katika Kata
  • Atakuwa Katibu wa Kamati  ya Maendeleo  ya Kata
  • Atakuwa mlinzi wa amani na msimamizi wa utawala bora katika Kata.
  • Atamsaidia Mkurugenzi kuratibu na kusimamia  shughuli za uchaguzi katika Kata.
  • Atamsaidia na kumwakilisha  Mkurugenzi katika kusimiamia maendeleo katika Kata.
  • Atasimamia utendaji kazi wa wataalam na watendaji wengine katika ngazi ya Kata.
  • Atakuwa mwenyekiti wa vikao vinavyohusisha wataalamu, watendaji wa Vijiji na NGO’katika  Kata yake.
  • Kuratibu na kuandaa taarifa za utekelezaji na kuziwasilisha kwa Mkurugenzi
  • Atakuwa msimamizi na mratibu wa takwimu zote zinazokusanywa katika Vijiji vya kata yake.
TGS C= TSHS. 309,800/= - 393,400/=
2AFISA MTENDAJI WA KIJIJI  DARAJA LA III (NAFASI 6)
  • Awe amehitimu kidato cha nne (IV) au sita (VI)
  • Awe na astashahada katika fani yoyote kutoka chuo chochote kinachotambulika na Serikali.
  • Atakuwa mtendaji na mshauri Mkuu wa Serikali ya Kijiji na kamati zake.
  • Atakuwa afisa Mhasibu wa Serikali ya Kijiji na atasimamia mapato na matumizi
  • Atakuwa katibu wa vikao /mikutano ya kijiji.
  • Atakuwa mlinzi wa amani katika Kijiji.
  • Atahamasisha  jamii kushiriki shughuli  za maendeleo katika Kijiji.
  • Atasimiamia maagizo yote ya Serikali yanayohusu maeneleo katika Kijiji.
  • Kuandaa taarifa za utekelezaji wa shughuli za serikali katika Kijiji na kuziwasislisha katika Kata /Wilaya.
TGS A/B = TSHS. 165,000/= - 193,700/= au  TSHS. 221,600/= - 278,300/=
3MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA LA  II (NAFASI 1)
  •  Awe amehitimu kidato cha  nne (IV) au sita (VI)
  • Awe na cheti cha utunzaji
     kumbukumbu
     katika  mojawapo
     ya fani za Afya,
     Masijala
     Mahakama na ardhi
  •  
  • Kutafuta kumbukumbu/nyaraka/ mafaili yanayohitajika na wasomaji.
  • Kuchambua, kuorodhesha na kupanga nyaraka katika makundi  kulingana na  somo husika kwa ajili ya matumizi ya ofisi.
  • Kuweka Kumbukumbu (barua, nyaraka n.k. ) katika mafaili.
  • Kushughulikia maombi ya   kumbukumbu/nyaraka kutoka taasisi za Serikali
TGS B/C TSHS. 221,600/= - 278,300/= au TSHS. 309,800/= - 393,400/=
4KATIBU MAHSUSI III (NAFASI 1)
  • Awe amehitimu kidato cha nne (IV)
  • Awe amehudhuria
      Mafunzo ya  uhazili
      na kufaulu
      mtihani wa Hatua
      ya Tatu.
  • Awe amefaulu
      somo la
      Hatimkato ya
      Kiswahili na
      kiingereza maneno
     80 kwa dakika
     moja.
  • Awe amepata
    mafunzo ya
    kompyuta kutoka
    chuo chochote
    kinachotambulika
    na serikali na
    kupata cheti  katika
    programu za
   Windows, Microsoft
   office, Internent, E-
   Maili na Bublisher.
    • Kuchapa barua, taarifa na nyaraka za kawaida.
    • Kusaidia kupokea wageni na kuwasaili shida zao na kuwaelekeza sehemu wanapoweza kushughulikiwa.
    • Kusaidia kutafuta na kumpatia Mkuu wake majalada, nyaraka au kitu chochote kinachohitajika katika shughuli  za kazi hapo ofisini.
    • Kusaidia kufikisha maelekezo  ya mkuu wake wa kazi kwa wasaidizi wake na pia kumuarifu kuhusu taarifa zozote anazokuwa amepewa na wasaidizi hao.
    • Kutekeleza kazi zozote atakazokuwa  amepangiwa na msimamizi wake wa kazi. 
TGS B = TSHS. 221,600/= - 278,300/=
5MSAIDIZI  WA OFISI
(NAFASI I)
  • Awe amehitimu  kidato cha nne
  • Awe amefaulu vizuri katika Kingereza , Kiswahili na Hisabati
  • Kufanya usafi wa ofisi.
  • Kutayarisha  chai ya ofisi
  • Kuhakikisha kwamba vifaa vya ofisi vinawekwa sehemu zinazostahili
  • Kupeleka mfuko wa posta nakuchuklua barua kutoka posta.
  • Kudurufu barua na machapisho kwenye kwenye  machine za kudurufia.
  • Kuweka katika majalada nakala za barua zilizochapwa  katika ofisi  aliyomo
  • Atachukua na kupeleka majalada na hati nyingine kwa  maafisa  wanaohusika na kuyarudisha baada ya kuafnyaiwa kazi.
  • Atatunza vifaa vya ofisi na kutoa ripoti kila vinavpoharibika .
  • Atafungua nilango na madirisha ya ofisi wakati wa asubuhi na kuyafunga wakati wa jioni baada ya masaa ya kazi. 
TGOS A = TSHS. 150,000/= - 211,200/=
6DEREVA DARAJA LA II  (NAFASI 3)
  • Awe na cheti cha mtihani wa kidato cha nne (IV)
  • Awe na leseni mpya daraja la C ya uendeshaji  magari
  • Awe na uzoefu wa kuendesha magari kwa muda usuopungua miaka  mitatu bila kusababisha ajali.
  • Awe na cheti cha majaribio ya ufundi daraja la II          (Trade Testgrade II)
  • Ataendesha magari ya ofisi.
  • Atahakikisha gari na vyombo vyake vipo katika hali nzuri wakati wote na kufanya uchunguzi wa gari kabla  na baada ya safari ili kugundua ubovu unaohitaji matengenezo.
  • Atafanya matengenezo madogo madogo katika gari
  • Atatunza na kuandika daftari la safari “Log book” kwa safari zote.
TGOS A = TSHS. 150,000/= - 211,200/=

MAMBO MUHIMU YA KUZINGATIA:
  • Barua zote za maombi  ziambatanishwe na vivuli vya vyeti halisi vya elimu na taaluma.
  • Nakala ya cheti cha kuzaliwa
  • Picha mbili (2) passport size za hivi karibuni
  • Maelekezo binafsi (Cirriculum Vitae)
  • Waombaji  wawe  na umri kati ya miaka 18 - 40
  • Waombaji walio kazini wapitishe maombi yao kwa  waajiri wao.
  • Mwisho wa kupokea maombi  ni tarehe 04/05/2012 saa 9:30 mchana
Aidha tangazo hili linapatikana kwenye tovuti ifuatayo: http://www.kilolodc.go.tz/
Kwa wakazi wa Mkoa wa Iringa matangazo haya yanapatikana katika mbao za matangazo kwenye ofisi za Halmashauri.

Barua zote zitumwe kwa,

MKURUGENZI MTENDAJI (w)
HALMASHAURI YA WILAYA YA KILOLO
S.L.P 2324
KILOLO.

No comments:

Post a Comment