Tuesday, December 15, 2015

BODABODA 901 WAHITIMU MAFUNZO YA USALAMA BARABARANI.BOFYA HAPA


 
Jumla ya waendesha vyombo vya moto 901 katika  tarafa za Bugene na Nyaishozi wilayani Karagwe mkoani Kagera  wamehitimu mafunzo ya usalama barabarani yalikuwa yanaendeshwa na taasisi  ya Future World Vocational Insitute kutoka Dar Es Salaam kwa kushirikiana na Jeshi polisi wilaya ya Karagwe.









 
Mafunzo hayo yaliyoanza tangu disemba 05 mwaka huu katika kata za Nyaishozi, Kayanga na  Bugene yamehitimishwa jana  huku wahitimu wa mafunzo hayo wakikabidhiwa vyeti na kutwakiwa kuzingatia waliyofundishwa ili kupunguza au kukomesha kabisa ajali za barabarani.












 
Akiongea wakati wa kufunga mafunzo hayo mkuu wa polisi wilaya ya Karagwe Mika Makanja alisema  mafunzo hayo waliyopata waendesha vyombo vya moto yatakiwa msaada kwao kama watayatumia inavyotakiwa na si vinginevyo.










 
Mkuu wa wilaya ya Karagwe Deodatus Kinawiro ambaye  alikuwa  mgeni rasmi katika ufungaji wa mafunzo hayo alieleza jitihada za serikali katika kushirikiana wadau wengine kuleta mafunzo kama haya ambayo anaamini kuwa yatakuwa msaada kwa waendesha vyombo vya moto na watumiaji wengine wa barabara.









No comments:

Post a Comment