Sunday, December 20, 2015

HAKI HUINUA NCHI NA UZALENDO NI VITENDO SIYO MANENO NA KUSOMA VITABU NI KUONGEA NA WATU WENYE AKILI NYINGI.



 
Wajumbe  wa  mabaraza  ya  Kata  wametakiwa  kuzingatia  haki  na  uzalendo  katika  kutoa  suluhu  na  hukumu  zao  wanaposikiliza   kesi  mbalimbali  zinazofikishwa  kwao  na  wananchi  wanaowazunguka  kwasababu  haki  huinua  nchi  na  uzalendo  ni  vitendo  na  siyo   maneno.






 
Wito  huo  umetolewa  na  mwanasheria   wa  halmashauri  ya  Kyerwa  Jovin  Rutainulwa katika   mafunzo  ya  siku  moja  ya  kuwezesha  mabaraza  ya  kata  wilayani  Kyerwa  yaliyofanyika  kwenye  ukumbi  wa  Western  Hotel amesema kuwa  wasipotenda  haki na  kuwa  wazalendo  wanaweza  kusababisha  malalamiko  mengi  kutoka  kwa  jamii na  wafanye  kazi  hiyo  kwa  uzalendo  mkubwa.










Amesema  kuwa  anatabua  kazi  kubwa  waliyonayo  pia  changamoto  nyingi  zinazowakabili  wajumbe  wa  mabaraza  hayo  zikiwemo  za  ukosefu  wa  vitendea  kazi  na  sehemu  za  kufanyia  kazi  lakini  hicho  kisiwe  kigezo  cha  kutotoa  haki  kwa  muda  muafaka  na  kushindwa  kuwasaidia  wananchi  waliowaamini kuwachagua.


No comments:

Post a Comment