Sunday, December 20, 2015

MWANAUME MMOJA APEWA ADHABU YA KUFANYA USAFI KWA MIEZI MITATU BAADA YA KUKUTWA AKIFANYA MAPENZI NA MBUZI WA JIRANI YAKE.BOFYA HAPA


 Mkazi  mmoja  wa kijiji  cha Keisangura  kata  ya  Nyamwaga wilaya  ya Tarime  mkoa  wa  Mara  amekamatwa  akijamiana  na  mbuzi.

Mwenyekiti  wa  kitongoji  cha  Malulu  Saimon  Mgacha  na  Kaimu  afisa  mtendaji  wa  kijiji  hicho  Mwita  Mseti   wamemtaja  aliyekamatwa  ni   Ntare  Nyambane  Ntare  mwenye  umri  wa  miaka  30




Baada ya  Mashauriano  yaliyofanyika  ofisi  ya  kijiji  hicho  yaliyohusisha  mmiliki  wa  Mbuzi  huyo Mwita Chongo wamesema  kitendo  kilichofanywa  na  mtuhumiwa  huyo  ni  kibaya  na  cha  aibu  kwa  jamii hivyo  wakaamua  kumpatia  adhabu  ya  kuchimba  shimo  la  choo  lenye urefu  wa  futi 12  pamoja  na  kufanya  usafi  kwenye  ofisi  ya  kijiji  kwa  kipindi  cha  miezi  mitatu.



Katika  utetezi  wake  mtuhumiwa  huyo Ntare Nyambane Ntare amesema  anaomba  msamaha  na  hajui  kilichomtokea  mpaka  kutenda  tukio  hilo  la  ajabu  kwani  anaye  mke  na  watoto  na  kukubali  kutimiza  adhabu  aliyopewa  na  viongozi  hao.

2 comments: