Monday, October 1, 2012

JAMANI TUWASAIDIE WATU HAWA NA KUWATHAMINI

Na: Mbeki Mbeki
      Karagwe

Jumla ya wanawake 450 walio wajane katika Wilaya ya Karagwe Mkoani Kagera wanakabiriwa na changamoto mbalimbali ikiwa ni pamoja na kukosekana msaada wa kisheria unaoweza kudai haki zao za msingi.
Hayo yalisemwa mwishoni mwa wiki na Mwenyekiti wa umoja wa wajane katika Wilaya ya Karagwe na Kyerwa Grace Mahumbuka wakati akizungumza na Habari Leo ofisini kwake.
Mahumbuka alisema kuwa wajane na watoto yatima wanajishughulisha na shughuli zao mbalimbali ili kupata kipato chao cha kukidhi ukali wa maisha, ambapo alisema huyang’anywa, hudhulumiwa, hudhalilishwa hata kubakwa na kushindwa kupata haki zao kwa kukosa asasii ya kisheria ya kuwasaidia.
Alisema kuwa vitendo vya kurithiwa kwa nguvu kindoa na mashemeji zao na baadhi ya wanajamii, watoto yatima wa kiume kulawitiwa na kuingiliwa kinyume cha maumbile kuwa vitendo hivyo vimechangia msongamano wa mawazo katika kundi hilo
 
Alisema kuwa kundi la Wazee,wajane na walemavu ni makundiyanayokabiliwa na changamoto za kutothaminiwa, kutoheshimiwa, kutosikilizwa na jamii na baadhi ya vijana kuwa watovu wa nidhamu ndani ya familia zao na jamii inayowazungunka.
Mahumbuka  alisema serikali ilitangaza kuwa wazee wote kupatiwa matibabu bure kuwa mpaka sasa serikali haijachukua hatua ya utekelezaji kikamilifu.
Aidha alisema Pensheni kwa Wazee kucheleweshwa na kutolipwa kabisa na kuongeza  kuwa pensheni  kwa wazee wakulima inayozungumzwa Bungeni na serikali kutotekelezeka.
Hata hivyo ameitaka serikali kutambua haki za msingi katika makundi hayo  na kuwafanya  kuishi kiusalama na kulindwa kwa mali zao ni pamoja na kupatiwa  bima ya afya kwa ajili ya afya zao.
 
 
 

No comments:

Post a Comment