Monday, October 1, 2012

JAMAN HII NI UTATA MTUPU ASILIMIA 40 YA WAKAZI WA WILAYA MPYA YA KYERWA NI WAHAMIAJI HARAMU.

Na Mbeki Mbeki.  
Kyerwa 
Mkuu wa Wilaya ya Kyerwa Mkoani Kagera Luteni Kanali (Mstaafu) Benedict Kitenga amesema Wilaya hiyo inakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo Uhamiaji haramu, uharibifu wa mazingira na mnyauko bacteria wa migomba.
Hayo yalisemwa jana na Mkuu wa Wilaya hiyo wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake.
Luteri Kanali (Mstaafu) Kitenga alisema kuwa Wilaya yake inakabiliwa na changamoto mbalimbali ambazo alizitaja  kuwa ni uhamiaji haramu ambapo alisema kuwa asilimia 40 ya wakazi wa Wilaya hiyo ni watu kutoka Uganda, Rwanda na Burundi.
Aliongeza kuwa katika kata ya Kibingo, Murongo, na Kaisho asilimia 70 ya wakazi wa kata hizo ni wahamiaji haramu kutoka  nchi jirani, aliongeza kuwa changamoto nyingine ni pamoja na uvuvi haramu, uharibifu wa mazingira ambao  umekithiri kwa kiasi kikubwa.
Alizitaja changamoto nyingine kuwa ni magendo ya Kahawa kwenda nje ya nchi  mnyauko bakteria wa migomba mnyauko fuzari unaoshambulia Kahawa uwindaji haramu na Ugonjwa wa  Ebora.
Pia kuwa Wilaya  hiyo inakabiriwa na changamoto ya utekaji wa magari ya abiria na migogoro ya ardhi kuwa vitendo hivyo visipodhibitiwa vinaweza kuharibu uchumi wa Wilaya na Taifa kwa ujumla.
Kitenga alisema kuwa uhamiaji huo haramu unaweza pia kuathiri  mradi  wa NIDA kuhusu utolewaji wa vitambulisho kwa watanzania kutokana na mwingiliano  wa watu kuwa mkubwa hasa kwa wilaya zilizo mpakani.

Aidha Mkuu huyo wa Wilaya alisema kutokana na Takwimu za sensa mwaka 2002 Wilaya hiyo ina wakazi zaidi ya laki nne na kuwa inasadikiwa kwa Sensa ya watu na makazi ya mwaka 2012, kwa ongezeko la watu kwa asilimia 2.9 idadi yao itakuwa ni zaidi ya laki sita.
 Hata hivyo amewataka wakazi  wa Wilaya hiyo kushirikiana na Serikali kudhibiti vitendo vya uhamiaji haramu, ambapo alisema  kuwa Mkoa wa Kagera unasadikiwa kuwa na wahamiaji haramu 18,000.

No comments:

Post a Comment