Na
Mbeki Mbeki
Karagwe.
Kwa upande wake, Mkuu wa shule ya Bugene Peter Mushumbusi ameipongeza bodi ya Kawosa kwa msaada wanayoitoa kwa watoto walio katika mazingira magumu na kuyataka mashirika mengine kujitokeza kutoa huduma kama hiyo katika jamii.
Karagwe.
Katika harakati za kupambana na changamoto
zinazowakabili wanafunzi walio katika mazingira hatarishi wanafunzi
175 Wilayani Karagwe wameweza
kulipiwa karo kutoka Karagwe Women Saccos (KAWOSA).
Akizungumza hivi karibuni na
waandishi wa habari katika shule ya Sekondari Ihembe Meneja wa Saccos hiyo
Goleth Elias alisema kuwa wamewalipia wanafunzi walio katika mazingira
hatarishi kiasi cha shilingi Milioni 35,000,000/= kwa ajili ya kulipia karo.
Elias alisema kuwa
wametoa fedha hizo ili kuwapunguzia makali ya madai waliyonayo na kuwapa moyo
wa kuendelea na masomo yao ambapo alisema kuwa baadhi ya watoto hao ni yatima
kutokana na wazazi kufa kwa kutokana na magonjwa mbalimbali ikiwemo ikimwi na
wengine wakiwa na wazazi wasio na uwezo
.
.
Meneja wa Saccos hiyo
alieleza kuwa wanafunzi hao wamekuwa wakikatisha masomo yao kutokana na kukosa
mahitaji muhimu ya shule ikiwa ni pamoja na kalamu vitabu, karo na matumizi
mengine ya lazima.
Alizitaja baadhi ya
shule za sekondari ambazo zimenufaika na fedha hizo kuwa ni Ihembe, Rugu,
Nyakasimbi, Nyakahanga, Bugene, Kayanga na Ndama na shule nyingine amezitaja
kuwa ni Ruhicho, Kiruruma Kawela, Kyabalisa, Nyabiyonza na shule ya Sekondari
Nono.
Aliongeza kuwa kutokana na uwezo wa ofisi yake kuwa
mdogo kila mwanafunzi amelipiwa shilingi 20,000/= ambapo pia mwaka jana
walilipiwa mahitaji ya darasani kutoka kwenye chama chao cha akiba na mikopo.
Naye, mwenyekiti wa
Saccos hiyo Safina Amrani amewataka wanawake wilayani humo kujiunga na saccos yao ili kuweza
kuinua vipato vyao kiuchumi, kuwa ongezeko kubwa la wanachama litasaidia chama
chao kuwa na uwezo mkubwa wa kukopesha na kutoa misaada kama hiyo.
Aidha amewashauri
wanafunzi walio pata msaada wa kulipiwa karo
kutumia fursa hiyo ili
kuwawezesha kukomboa maisha yao kwa baadae.
Kwa upande wake, Mkuu wa shule ya Bugene Peter Mushumbusi ameipongeza bodi ya Kawosa kwa msaada wanayoitoa kwa watoto walio katika mazingira magumu na kuyataka mashirika mengine kujitokeza kutoa huduma kama hiyo katika jamii.
Hata hivyo, amewataka
wanafunzi walionufaika na fedha hizo kusoma kwa bidii ili baadae waweze
kuwasaidia watoto wengine wenye hali kama hizo ambapo pia alisema waachane na
makundi ya kihuni, ulevi, na uvutaji bangi kuwa yanaweza kuhatarisha maisha
yao.
No comments:
Post a Comment