Thursday, June 27, 2013

CHANGAMOTO YA ELIMU YA IKABILI KARAGWE

KARAGWE
     Halmashauri ya wilaya ya Karagwe mkoani Kagera inakabiliwa na changamoto mbalimbali katika sekta ya Elimu ikiwemo upungufu wa miundo mbinu ya vyumba vya madarasa na nyumba za walimu.
 
     Hayo yalibainishwa jana na Katibu wa mfuko wa Elimu Leofanston Lwangoga ambaye pia ni kaimu katibu wa chama cha Walimu (CWT) wilayani Karagwe wakati alipokuwa akisoma taarifa ya kikosi kazi cha elimu (Karagwe education task force) kwenye mkutano wa wadau wa elimu wilayani humu.
 
     Lwangoga akisoma taarifa hiyo alisema kuwa changamoto zinazoikabili sekta ya elimu wilayani kwake ni pamoja na upungufu wa miundo mbinu ya vyumba vya madarsa,nyumba za walimu, maktaba, mabweni, maabara na majengo ya utawala.


     Alizitaja changamoto nyingine kuwa ni pamoja na kutokuwepo kwa samani za kutosha kama meza, madawati na kabati ambapo aliongeza kuwa Ikama ya walimu kutotosheleza mahitaji , upungufu wa vitaqbu vya kufundishia na kutotosheka kwa mlo wa mchana kwa wanafunzi walio wengi kwenye shule za msingi na sekondari.


     Alibainisha baadhi ya mapungufu katika sekta hiyo kuwa ni vyumba vya madarasa 857, kuwa vilivyopo ni 872 na vinahitajika 1729 katika shule za msingi huku nyumba za walimu zikiwa na upungufu 1449 zilizopo 309 na zikihitajika 1758.


     Katika shule za sekondari alisema kuwa vinahitajika vyumba 73, vilivyopo ni 60 na kuna upungufu wa vyumba 13, ambapo aliongeza kuwa nyumba za walimu zinahitajika 300 zilizopo ni 32 na kuna upungufu wa nyumba 267.
     Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri hiyo Bosco Nduguru alikiri kuwepo kwa changamoto hizo na kuongeza kuwa wananchi walio wengi hawatambui kuwa wao ni wamiliki wa shule hali inayosababisha washindwe kuchangia elimu na kuwachukua wazazi wenye watoto shuleni.


     Nduguru alisema changamoto nyingine ni bodi na kamati za shule kutotambua majukumu yake hali inayosababishwa na kamati hizo kutopewa mafunzo ya mara kwa mara, kuwepo kwa utoro wa rejareja na kudumu walimu na wanafunzi na watendaji wa kata na vijiji kutowajibika ipasavyo katika kusimamia masuala ya elimu kwenye maeneo yao.


     Alisema changamoto hizo zimetokana na utafiti uliofanywa na timu ya wajumbe saba toka miongoni mwa wajumbe 16 wa kikosi kwake cha elimu kilichoteuliwa na Mkuu wa wilaya septemba mwaka jana.


     Baadhi ya wadau wa elimu waliohudhuria katika mkutano huo walisema kuwa kila mdau wa elimu na mwananchi kwa ujumla analo jukumu la kuchangia Elimu na mwananchi kwa ujumla analo jukumu kuchangia elimu kifedha ili kuinua kiwango cha elimu wilayani humo ambapo ulibuniwa utaratibu wa kubaini wachangiaji uhamasishaji jamii, uandaaji na usambazaji wa vitabu vya makusanyo na uchangishaji.


     Walisema kuwa fedha itakayo kusanywa itagawanywa kurudishwa kwenye kata kulingana na kiwango kitakachokuwa kimewasilishwa na kata husika kwa kuzingatia asilimia zitakazowekwa ambapo wakusanyaji wakuuu wa michango hiyo ni maofisa watendaji wa kata wakisaidiana na watendaji wa vijiji.


     Aidha walipendekeza fedha hizo baada ya kukusanywa zigawanywe kw uwiano asilimia 60 zipelekwe kwenye kata kwa ajili ya maendeleo ya elimu, asilimia 30 zipelekwe mfuko wa elimu na asilimia 10 ziingizwe kwenye mfuko wa Halmashauri kwa ajili ya dharula kama vile maafa.


     Hata hivyo wameitaka Halmashauri hiyo kufanya mkakati huo kuwa endelevu kuanzia April hadi mwaka huu ambapo walisema kiasi cha shilingi 2,465,7000,000 kinahitajika katika kukabiliana na changamoto hizo.
 
 






No comments:

Post a Comment