Thursday, September 19, 2013

KIPAO MBELE CHA KWANZA ,CHA PILI NA CHA TATU NI ELIMU KUWEKEZA NI MUHIMU KWA KILA MTU.


 Na
      Juhudi   Felix
      Karagwe

Watanzania wametakiwa kuwekeza katika elimu kutokana na mabadiliko na maendeleo ya kiuchumi, kisiasa na kiteknolojia ndiyo yanayofanya ulimwengu kubadilika kwa kasi kubwa

Hayo yalisemwa jana na Kamishina wa Polisi Saimoni Siro  katika  hotuba ya uzinduzi rasmi wa shule ya msingi Kazoba akimwakilisha Waziri wa mambo ya ndani Daktari Emmanueli Nchimbi aliyekuwa amealikwa  kama mgeni rasmi katika hotuba iliyosomwa  Kayanga  wilayani Karagwe mkoani Kagera.

Siro alisema kuwa wananchi hawana budi kuwekeza katika elimu kutokana na mabadiliko na maendeleo ya kiuchumi, kisiasa  na kitechnolojia ndiyo yanafanya ulimwengu kubadilika kwa kasi kubwa ambapo aliongeza kuwa kila binadamu anayetaka kuishi na kupata mafanikio kuendeana na mabadiliko hayo.

Katika hotuba hiyo alisema kama ambavyo wengi wao wanafahamu hali ya dunia inabadili kila kukicha kuwa dunia miaka hamsini iliyopita ni tofauti sana na dunia hali kadhalika dunia ya miaka hamsini ijayo itakuwa tofauti ilivyo sasa.

Alisema elimu ndiyo  msingi kwa kuendana na kazi ya mabadiliko yanayotokea nchini na duniani kote kuwa lazima kila mmoja wao bila kujali umri, jinsi au hadhi yake awe tayari kujifunza kila siku.

Alieleza kuwa kwa watoto wao elimu bora ndiyo urithi  wenye maana ambao utawafanya waweze kukabiliana na changamoto za kimaisha katika dunia ya kisiasa inayoongoza na teknolojia.

Alisema ili kufanikiwa kiuchumi kijamii na kisiasa ni lazima wawe na elimu bora itakayowawezesha kujiamini kitaifa na kushirikiana kwa manufaa  yao na nchi yao kuwa msingi wa kujiamini unatokana na elimu bora inayotolewa katika mazingira bora kama ya shule hiyo.

Siro alisema uwekezaji huo ni kielelezo cha utashi wa  wamiliki wa shule hiyo kujua changamoto zinazowakabili kitaifa na kimataifa kutokana na ukweli kuwa hali ya elimu yao bado siyo kuridhisha sana.

Alisema ni lazima wakubali kutoka katika hali hiyo ya kuwapeleka nje ya nchi na badala watafute suluhisho la matatizo yao elimu kwa kuwekeza katika miundo mbinu.

Alifafanua kuwa ni vema watu wenye uwezo kiuchumi wakirie kuwekeza katika sekta nyingine za kiuchumi unapaswa kuendana na uwekezaji katika elimu kuwa madhara ya kutowekeza katika elimu ni pamoja na kuwafanya watoto wao nje ya soko la ajira kwa kukusanya uwezo wa kushindana na uwezo wa mataifa ya nje.

Aliongeza kuwa  shule hiyo iendelee kuzingatia na kuwafundisha  maadili mema kwa watoto kujali utu mshikamano na uzalendo kwa taifa lao kuwa elimu bila maadili haitasaidia sana kama taifa.

Katika hatua nyingine Siro alisema nchi inayochangamoto kubwa ya usalama hasa katika mikoa ya mipakani hasa kubwa na uhalifu hasa ujambazi na utekaji wa magari uvamizi wa mapori hivyo uliwataka wananchi  kushirikiana na serikali kudhibiti matendo hayo haramu.

Kwa upande wake mkurugenzi wa shule hiyo James Peter Kazoba alisema kuwa shule hiyo ni pekee katika mkoa wa kagera inayofundisha masomo ya kifaransa ilianza mwaka 2008 ikiwa na jumla ya wanafunzi 7 tu.


Kazoba alisema shule hiyo ni ya mchipuo wa lugha ya kiingereza darasa la kwanza hadi la saba na gharama ya shilingi bilioni moja zimetumika katika uwekezaji wa ujenzi wa majengo ya shule hiyo.

Aidha katika uzinduzi wa shule uliohusisha pia maafari ya darasa la saba wanafunzi wavulana 5 na wasichana 15 wamehitimu darasa la saba mwaka huu kwa mara ya kwanza ambapo shule hiyo ikiwa ni ya tatu katika ufaulu wa mtihani wa majaribio darasa la saba kati ya shule 212 za wilaya hiyo.

Hata hivyo alizitaja changamoto mbalimbali zinaikabili shule hiyo binafsi ya kutwa na bweni kuwa ni pamoja na ukosefu wa bwalo la chakula, jiko na baadhi ya wananchi kuvamia ardhi ya shule.


No comments:

Post a Comment