Saturday, September 14, 2013

Wazazi wapewa somo



 Na
    Juhudi   Felix

BUGENE –KARAGWE
Wazazi na walezi wametakiwa kutoa fursa sawa kwa watoto wao kupata  elimu kuliko kutoa upendeleo kwa watoto wa kiume tu kwani  elimu ndio uwekezaji muhimu wa mkobozi wa mtu yeyote bila kujali jinsia yake.

Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa mkoa wa Kagera Kanali mstaafu Fabiani Massawe ambaye alikuwa mgeni rasmi katika mahafari ya sita ya kuwaaga wahitimu wa darasa la saba katika shule ya kiingereza ya Mtakatifu Peter Claveri wakati akihotubia wanafunzi,wazazi na wageni waalika katika mahafari hayo.
Amesema kuwa elimu ndio ukombozi pekee kwa mtu yeyote,hivyo na kuwataka wazazi kutokuwa na dhana ya kusema kuwa watoto wa kike hawana msaada wowote kumbe hali ni tofauti kwani watoto wa kike ndio wanaosaidia wazazi wao zaidi kuliko watoto wa kiume.

Huku akitolea mifano mbalimbali ya baadhi ya wanawake waliofanikiwa kushika nafasi za juu za uongozi  miongoni mwaoni spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano w Tanzania Anna Makinda ,Rose Migiro ambaye alikuwa naibu katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa na mkuu wa wilaya ya Karagwe kuwa hawakupewa nafasi hizo kwa upendeleo bali wamesoma ndio maana wakashika nafasi hizo.

Amewataka pia wahitimu kuwasaidia wazazi katika kipindi chote watakachokuwa wanasubiria matokeo yao ya mtihani walioufanya wa kuhitimu  elimu yao ya msingi,na kuwataka kutojihusisha matendo maovu  kwani wamelelewa katika maadili mema ya dini hivyo kuyaendeleza wakati wote wa maisha yao ili kuyafikia malengo yawliyonayo.

Amewataka pia walimu kuzidisha malezi yao ya awali ili kuendeleza heshima na hadshi ya kazi hiyo kwani kipindi cha nyuma mwalimu aliheshimiwa sana katika jamii na walitunzwa bila gharama  kutokana na kutimiza wajibu wao tofauti na hivi sasa ambapo mwalimu amepoteza hadhi yake kutokana na kutotimiza wajibu wake sawasawa  kama ilivyokuwa mwanzo.

Amelishukuru kanisa  na taasisi zake kwa kuendelea kutoa huduma kwa jamii hivyo kuisaidia serikali katika jitihada za kuhudumia jamii kikamilifu,na kuongeza kuwa katika mtihani wa kumaliza elimu ya kidato cha nne shule zinazomilikiwa na kanisa ndizo ziliongoza kwa matokeo mazuri huku akitolea mfano shule ya mtakatifu Franciss ya mkoani Mbeya iliyoshika nafasi ya kwanza kitaifa.

Aidha,katika mhafari hayo kumefanyika harambee ya kuchangia ujenzi wa sekondari ya Mtakatifu Peter Cleveri ambayo inatarajiwa kujengwa  eneo la Kihanga kuanzia mwaka wa 2014  ambapo  eneo la heka 33.69 tiyari limeishapimwa kwa ajili ya ujenzi.Katika harambee hiyo kiasi cha pesa Taslimu 598,200 zilipatikana huku ahadi ikiwa ni sh 5,170,000 jumla ya  ahadi na taslimu ni sh  5,768,200.

Wahitimu wa mwaka huu ni jumla ya wanafunzi wapatao 32  kati yao wanafunzi wa kiume ni 19 na wanafunzi wa kike ni 15 ambapo ni mahafali ya sita tangu shule hiyo  kuanzishwa na kujivunia kuwa na ufaulu mzuri ndani ya wilaya mkoa hata Taifa kwa ujumla.

Hata hivyo amewataka wananchi kuwekeza zaidi katika elimu kwani ndio pesheni ya uzeeni iliyobakia  kwa maana wazazi kipindi hicho huwa wameishiwa nguvu za uzalishaji mali na watoto wao ndio watakao wasaidia kuwatunza.

No comments:

Post a Comment