Bodi za shule
binafsi zahimizwa kusimamia
nidhamu za watumishi
Na Shaaban Ndyamukama
Bodi ya shule ya sekondari ya RHEC English Medium iliyoko wilaya ya Ngara
mkoani Kagera imetakiwa kujiamini na kusimamia nidhamu ya shule na watumishi
kwa kukaa vikao hatimaye kutatua
migogoro kati ya utawala na watumishi
ili kuepuka hasara kwa shule wanafunzi na wazazi wao
Hayo yamebainika jana katika mkutano wa wazazi na uongozi wa bodi ya shule hiyo wakati wa
kupokea taarifa ya ajali ya moto ulioteketeza mali zote za wanafunzi katika
vyumba viwili vya bweni la wasichana lenye uwezo wa kulaza wanafunzi 80 wiki
iliyopita wilayani Ngara.
Mmoja wa wazazi
katika mkutano huo Bw Josiasi Kimuga amesema kuwa bodi ya shule inayoongozwa na Mwenyekiti wa
kamati ya huduma za jamii katika halmashauri ya wilaya ya NgaraThomson
Seyongwe kijisimamia na kutoa maamuzi
kuliko mtu mmoja au kundi la watu
wachache na kukwamisha utoaji wa taaluma
katika shule yake
Bw Kimuga amesema
kuwa kukosekana kwa vikao vya kutatua migogoro na kutoa maamuzi kumesababisha
hata kukosekana muhtasari wa mkutano wa wazazi na bodi mwaka jana ambao
ulitakiwa kutunzwa na katibu ambaye ni
mkuu wa shule. Alisema kuwa migogoro iliyopo shuleni isipotatuliwa haraka wazazi watapoteza
wanafunzi wao kitaaluma au hata kuwapotezea maisha na wajumbe wa kamati ya
shule ya msingi na bodi ya sekondari
wasimamie majukumu yao
kwani ndio wanaowakilisha wazazi
Akitoa taarifa ya moto Mkuu wa shule hiyo Bw Venanti
Verdiani amesema moto uliounguza bweni la wasichana ilisababisha hasara kwa mali za wanafunzi na shule kwa thamani ya shilingi miliono 152.48
Alisema katika ajali
ya moto huo nusu ya bweni lenye vyumba viwili viliteketea na mali za wanafunzi
zenye thamani ya shilingi milioni 14.6
, vitanda 72 viliungua vinavyokadiliwa kwa shilingi kwa Tsh milioni 9.79 na bweni lenyewe nusu iliungua na ukarabati
wake pekee utagharimu Tsh milioni 45.36
Alisema kuwa juhudi za haraka zilifanyika ambapo wasamalia
wema na uongozi wa shule ni waliweza kutoa magodoro na mavazi pamoja na
mahitaji mengine ya kila sikukwa wanafunzi waliounguliwa bweni lao na thamani
yake ni Tsh. mil 18.4
Alisema kuwa utafiti
wa kujua chanzo cha moto unaendela kufanyika chini ya vyombo vya dola likiwemo
jeshi la polisi na wanafunzi wote 15 waliokuwa wamelazwa katika Hospitali ya
Rulenge wilayani humo kwa mshituko waliruhusiwa baada ya afya zao kurejea
katika hali yao
ya kawaida na amewashukuru wakazi wa Rulenge na wauguzi kwa msaada walioutoa
kuokoa maisha ya wanafunzi
Kwa upande wake Meneja wa shule hiyo Helena Adriani ambaye
ni Mwenyekiti wa CCM wilayani Ngara alitoa hali halisi ya migogoro ya shule
hiyo kuwa ni walimu upande wa wa shule ya msingi kuwa na utovu wa nidhamu hali
iliyosababisha hata wengine kupigana shuleni
na kumwaga chakula cha wanafunzi wao
Alisema kuwa walimu hao walikuwa hawafundishi kwa kuanzisha
migomo baridi na kuwafanya wanafunzi kukosa zaidi ya mada katika masomo ambapo
juhudi za haraka zilifanywa na walimu wa sekondari kufundisha wanafunzi wa
shule ya msingi hadi usiku
Alisema baadaya kuwepo uvunjifu wa amani katika shule yake
aliwaodoa kazini walimu saba na watumishi wengine watatu tarehe 03 mwezi huu na siku chache ndipo bweni
likaungua na kusababisha hasara kubwana yeye alikuwa safarini mkoani Dodoma
Aidha Meneja huyo alisema changamoto nyingine katika shule
hiyo ni ukosefu wa fedha za kutekeleza miradi mbalimbali kama
kujenga uzio kupata huduma bora ya maji kwa wanafunzi kwani michango ya shule
ndiyo inayosaidia kuleta maendeleo ya shule yake
‘Nawasihi wazazi kulipa karo kwa wakati na katika kufunga
muhula wa kwanza Aprili mosi mwaka huu watakaokuwa bado kulipa karo
nitawafukuza sitawapokea muhula wa pili mwezi mei kwani walimu wanahitaji mishahara na gharama
za chakula kulisha wanafunzi zimepanda sana’.Alisema
Meneja
Hali hiyo ilimfanya Mbunge mtaafu Angas Gwassa Sebabili
kuutaka uongozi wa shule kuweka uzio na walinzi wenye sifa watakaolinda mali za
shule na maisha ya wanafunzi Sebabili aliwataka
wazazi kulipa fedha za michango mbalimbali na karo kuwaandaa watoto wao
kukabiliana na ushindani wa kielimu na uchumi katika shirikisho la Jumuia ya
Afrika ya Mashariki vinginevyo watakuwa watazamaji na vibarua kwa watakao toka
nchi nyingine wanachama wa shirikisho la jumuia hiyo
Alisema wanaotafuta elimu kwa sasa ni gharama na zile shule
za serikali taaluma yake haiko katika mfumo wa kupata ajira bali inawaandaa
wananchi wake kuwa watawaliwa kwa kuwapa elimu isiyoweza kuwaingiza kwenye
ushindani na utandawazi uliopo
‘Elimu ndiyo dira ya kumkomboa mwanajamii yeyote duniani kama
mtapuuzia kutoa michango au kulipa karo kwa wanafunzi nyie ndio mtakaojuta na
watoto wenu kuishi nao nyumbani wakiwa watu wazima’.Alisema Sebabili
Wazazi wameshauri ujenzi wa bweni utakaofanyika uweke
miundombinu ya kukabiliana na majanga na majengo ya bweni yasiwekewe nomdo
katika madirisha na milango ya kufungia kwa nje kwani ili kuepukana na hatari
ya kupoteza maisha ya wanafunzi
Shule ya RHEC English Medium ina wanafunzi 617 kati ya hao 324 wanasoma sekondari na 293
ni wanafunzi wa shule ya msingi ambapo kwa sasa imejengewa uzio uliofikia hatua
ya nusu ya eneo la shule kwa gharama ya Shilingi milioni 7.52
No comments:
Post a Comment