Thursday, April 19, 2012

HII NI KUTOKA NGARA -MKOA WA KAGERA

WANANCHI  WILAYANI NGARA  WAJENGEWA ZAHANATI NA  HDT  KAGERA

 
Shirika ka HDT lenye makao makuu jijini Dar es Salaam  limetoa msaada wa jengo  la zahanati katika kijiji cha Mumuhamba  wilaya ya Ngara mkoani Kagera lenye  thamani ya TShilingi milioni  50.5
Akikabidhi jengo hilo  April 17  kwa uongozi wa Halmashauri ya wilaya ya Ngara kwa niaba ya mkurugenzi wa HDT DR Peter Bujari  Afisa miradi wa shirika hilo la Human Development Trust  (HDT) mkoaniKagera  mchungaji Feres Sendegeya alisema HDT  imejenga zahanati katika kijiji hicho  kwa kushirikiana na shirika rafiki la heath of Australi and Tanzania (HAT)
Mchungaji sendegeya alisema kuwa mradi wenyewe kwa kujenga zahanati umegharimu shilingi milioni 49,na laki moja  kati ya hiz shilingi ilioni 35.5 sawana asilimia 81 zimetumika kujenga
Alidai  kuwa katika ,usimamizi na ukaguzi ni kiasi cha shilling milioni nne sawa na asilimia tisa na utoaji wa mafunzo kwa kamati za afya ya kijiji na wahudumuwa afya ya msingi jumla shilingi milionio 3.7 sawa na 7% na hadi kukabidhi mradi umekamilika kwa kiasi cha shilingi Mil 50.5  hamsini 
Alisema kuwa HAT ndiye mfadhili   na  HDT  ilisimamia ujenzi kwa lengo la kusaidia wananchi kuboresha huduma za kijamii na hadi jengo hilo linakamilika wananchi kwa kutumia nguvu zao hasa kukusanya vifaa vinavyopatikana kwenye mazingira yao  thamani yake ni kati ya shilingi milioni mbili na laki tano
Aidha aliongeza  kwa kusema kuwa  zahanati hiyo itahudumia wananchi wapatao 5,076 wa kijiji cha Mumuhamba na kati ya hao wanawake ni sawa na 54% ambao ni kipaumbele cha taifa katika malengo ya millennia
‘Tunaaminikwa hatua hii itasaidia malengo ya millennia katika utekelezaji wa program ya MMAM  na shirika litaendelea na miradi ya afya katika kijiji hiki  maana uwepo wa zahanati hii shirika litawasiliana na Halmashauri ya wilaya kuondoa changamoto mbalimbali’.Alisema  Mchungaji Sendegeya
 Akitoa shukrani kwa niaba ya serikali ya wilaya ya Ngara na wananchi wa kata ya Bukiriro kilipo kijiji cha Mumuhamba Mwenyekiti wa Halmashari ya wilaya ya Ngara John Shimilimana  aliwasihi wananchi kuilinda miradi  inayoletwa na wafadhili pamoja na serikali kwani mara inapokamilika  inakuwa ni mali yao
Alisema kuwa ili wananchi wapate huduma za afya kila kaya ijiunge na bima ya mfuko wa afya ili fedha zao ziweze kutumika kununua dawa kwa haraka huku serikali ikisaidia kuongeza kiwango cha  michango yao kwa asilimia hamsini .Alisema mara baada ya miundombinu itakapokamilika kama nyumba ya kuishi waganga na wauguzi choo cha wagonjwa na wafanyakazi wengineo  halmashauri itakuwa tayari kuwaleta watumishi toka idara ya afya kwa ajili ya kuwahudumia wananchi.
Alisema kuwa endapo wananchi wataendelea kujitolea kwa kukusanya zaidi vifaa  vya ujenzi halmashauri itaharakisha kutoa nguvu zaidi kuwaunga mkono katika kuhakikisha changamoto zilizoko zinaondoka katika kijiji hicho na maeneo ya jirani na kuwapunguzia mwendo mrefu akina mama wajawazito na watoto chini ya miaka mitano kutafuta huduma mbali na maeneo yao

 
 Kwa upande wake Diwani wa kata ya Bukiriro  Emily Nkilamachumu alisema halmashauri ya wilaya isichelewe kuleta wataalamu wa afya kuhudumia wananchi kwa kuwa vifaa viko tayari na fedha za kusogeza hadi eneo la ujenzi zimeshatolewa na wananchi wa kijiji hicho. Alidai kuwa wananchi licha ya kuchangia na kufikia hatua ya jengo kukamilika changamoto iliyopo ni kupata watumishi wa afya waadilifu wenye kujali maslahi ya wananchi hivyo halmashauri kupitia ofisi ya Mganga mkuu wa wilaya iwatume wafanyakazi wa afya walio na moyo wa kujituma katika kutoa Huduma na wenye kuzingatia kanuni za utumishi.
        Wananchi wa kijiji cha Mumuhamba kabla ya kujengewa zahanati hiyo walikuwa wakilazimika      kutembea umbali wa kilomita tano hadi kumi kutafuta Huduma za Afya katika kituo cha Afya cha kata ya Bukiriro na wengine walikosa dawa kwa kuwa na changamoto za kukosekana  katika rejesta ya watumiaji wa kituo hichokinachohudumia kata nne za tarafa ya Rulenge Ngara
Mkurugenzi wa Shirika la  HDT Dr Peter Bujari ambaye ni mzaliwa wa wilay ya  Ngara alianzisha shirika hilo kwa lengo la kutoa Huduma za kijamii na mpaka sasa limepanuka na kuhudumia baadhi ya jamii katiak mikoa ya mbeya Ruvuma na kagera hasa kusaidia watoto na wanawake walio katika mazingira hatarishi
Watoto hao na wanawake hupata msaada wa  mitaji ya kuinua maisha yao ikiwa ni pamoja na kusomesha watoto wa shule za msingi na sekondari walio katika mazingira magumu kwa kupewa vifaa vya kujifunzia huku walezi wao wakipewa mbinu za ujasiliamali kupunguza umaskini katika familia .
Katika mkoa wa kagera shirika hilo linatoa Huduma katika wilaya za Bukoba muleba karagwe Ngara na Biharamulo ikiwa ni pamoja na kusaidia waathirika wa VVU kwa kuwapa dawa za kuzuia magonjwa nyemelezi na mbinu za kuwaongezea matumaini ya kuishi na kujumuika na jamii katika shughuli mbalimbali.
Kwa sasa wigo wa Huduma kwa shirika hilo umepanuka na kujumuisha kata nane wilayani Ngara ambazo ni Bukiriro, Rulenge ,Rusumo ,Kabanga, Bugarama, Nyakisasa, Muganza na Murusagamba ambapo baadhi ya familia hupewa mifugo na kuitunza kusomesha watoto na familia nyingine hupewa fedha taslimu kila kaya shilingi laki moja ili kuwa wajasiliamali.

No comments:

Post a Comment