Thursday, April 19, 2012

NGARA NAO KWA UDOKOZI MIE SIMO


Watiwa mbaroni kwa udokozi katika duka wilayani Ngara

Vijana wawili wakazi wa mji mdogo wa Rulenge wilaya ya  Ngara mkoani Kagera wamenusurika kuuwawa na wananchi wenye hasira kali baada ya kudokoa bidhaa kwenye duka la mjasiliamali katika mji huo  jumatatu wiki hii 
  Vijana hao ni Shabani Jacobo ( 37) na Godfrey Turbo (27 ) waliingia katika duka la mfanyabiashara Ismail Mulengera  wa mji  wa Rulenge kutafuta bidhaa kuwaletea wateja wake na walipofika ndani ya stoo walianza kukwepesha baadhi ya mali na katika kuficha ndipo wakabambwa na mwenye duka
Wananchi waliowakamata  waliwakuta na katoni mbili za sabuni na makasha mawili ya amila aina ya pasha na kuanza kupata kipondo kabla ya madhara kutokea kwao waliokolewa na polisi jamii kituo cha Rulenge  kwa  kufungwa kamba katika  kuokoa maisha yao na kufikishwa  kituo cha polisi
Akiongea na mwanahabari aliyefika eneo la tukio mmiliki wa duka walikodokoa vijana hao ismail mulengera amesema kuwa amekuwa akiwaamini kwa kushusha bidhaa katika magari atokapo kahama lakini kila akifanya majumuisho ya mauzo amekuwa akipata hasara ya mali aliyonunua

 ‘’Si mimi  pekee katika mji huu kuwatumia hawa wabeba kago bali wamekuwa wakitumiwa na hata wenzangu pia  ni ndugu zetu lakini kwa tabia hii hakuna kuwalea watatutia hasara’’. Alisema Mulengera
Naye mwenyekiti wa mji huo  Saidi Kiveve alisema kuwa vijana hao ni hohe hahe na hivyo mwenye duka apunguze jazba na kuwasamehe kwani  thamani ya mali waliyokutwa nayo ni ndogo
‘’Hawa ni vijana wa hapa na kama ismaili ni Mwislamu anapaswa kuwasamehe na sisi viongozi wa kijiji kuwaonya si kuwafungakama hasira zinavyomtuma’’.Alisema mwenyekiti Saidi
Mkuu wa kituo cha polisi cha rulenge ambaye hakutaka jina lake litajwe gazetini amethibitisha kuwapokea vijana hao na kwamba uchunguzi dhidi ya tuhuma zinazowakabili utafanyika.Ends

No comments:

Post a Comment