Ng’ombe 400 kutoka Rwanda wakamatwa wilayani Ngara
Na Shaaban Ndyamukama
Maofisa waandamizi wa halmashauriya wilaya ya Ngara Mkoani
Kagera wamenusurika kuuawa na Kundi la wafugaji wanaodaiwa kutoka nchi jirani
ya Rwanda wakati wa zoezi la kusaka Ng’ombe ambao hawajapigwa chapa ya alama ya
Tanzaniawalioko wilayani humo
BAADHI YA NG'OMBE WALIOKAMATWA KTK MSAKO HUO
Maofisa hao wa serikali walilazimika kutimua mbio kunusuru
maisha yao baada ya wafugaji hao wanaoendesha shughuli zao katika pori la
kimisi lililoko kwenye wilaya za Ngara
na Karagwe, kuwakimbiza huku wakiwa na bunduki aina ya SMG yenye magazini
ya risasi 30.
Tukio hilo limetokea jumamosi Machi 31 wakati maofisa hao wa
serikali wakiongozwa na Afisa mifugo wa wilaya ya Ngara Dr Richard Ngowi na Afisa
tafara ya Nyamiaga Bw Godian Bagambweki, wakifanya msako dhidi ya mifugo iliyoko wilayani humo kinyume cha
sheria
“Tulipofika katika kitongoji cha Kaumuli kata ta Kasulo,
tulikamata kiasi cha ng’ombe 400 ambao wanasadikiwa kutoka nje ya nchi na
ng’ombe hao ni mali ya Medard Muhutu Mudei raia kutoka Rwanda ambao
tuliwakamata kwa kuwa hawana chapa inayowatambulisha kama Ng’ombe wa Tanzania.
be 200”, alisema Dr Ngowi
Alisema wachungaji wa ng’ombe wengine 200 mali ya Bw Jackson
Venant ambaye naye anadaiwa kuwa
mwenyeji wa Rwanda, walichuka silaha za ina mbalimbali ikiwa ni pamoja a
bunduki aina ya SMG na kuanza kuwatishia
“Kundi la wachungaji wanaofikia 18, wakiwa na mapanga,
marungu na Bunduki walianza kututishia, askari mgambo sita ambao walikuwa
wamefuatana nasi bila silaha walianza kukimbia na sissi tukafuata”, Alisema Dr
Ngowi
Alisema walilazimika kuacha ng’ombe hao na kwenda kuomba
msaada kwa askari polisi walioko kwenye kizuizi cha barabara inayotoka Ngara
kuelekea Karagwe, ambapo wachungaji hao walirejea porini baadaya kuwaona askari
polisi.
Dr Ngowi amesema kwa mujibu wa sheria ya magonjwa ya mifugo
namba 17 ya mwaka 2003, kila mmiliki anapaswa kutozwa faini isiyoipongua
shilingi milioni mbili kwa kosa la kuingiza nchini mifugo ambayo haina chapa ya
Tanzania.
Aidha amesema wamiliki hao wanapaswa kutozwa faini ya shilingi elfu
50 kwa kila ng’ombe kwa kuharibu
mazingirra ya halmashauri husika
Kwa muda mrefu maeneo ya mapori ya wilaya za mkoa wa kagera
yamevamiwa na wafugaji kutoka Rwanda na Burundi, maelfu ya mifugo na kusababisha
madhara mbalimbali ikiwa ni pamoja a uharibifu wa mazingira
Katika hatua nyingine
Afisa tarafa ya Nyamiaga Bw Godian Bagambweki ambaye alishiriki katika msako
huo wa ng’ombe amedai kushuhudia mizoga ya Tembo 12 katika pori la kimisi ambao
waliuawa na watu wanaosadikiwa kuwa majangili ambao waliondoka na meno ya tembo
hao
“Mizoga hiyo ya tembo nimeishuhudia jirani na zizi la Bw
Jackson anayeishi kweye pori hilo. Kama serikali tunatakiwa kujipanga na
kuchukua hatua zaidi dhidi ya watu wenye mifugo katika mapori ya hifadhi”
.Alisema afisa tafara huyo
Mwezi June mwaka jana wakazi sita wa kijiji cha Murubanga
wilayani Ngara wanadaiwa kuuawa na wafugaji kutoka nje ya nchi wakati wananchi
hao wakipinga hatua ya ng’ombe wa wafugaji hao kulisha katika mashamba yao
Akizungumzia tukio hilo la siku hiyo Mkuu wa wilaya ya Ngara
Kanali Mstaafu ameliagiza jeshi la
Polisi kumtafuta na kumkamata mfugaji
huyoJackson Venant ili aweze kufikishwa
kwenye mikono ya sheria
Akiongea katika eneo la Kata ya Kasulo baada ya kupata
taarifa hizo, kanali Nyakonji alisema idara ya uhamiaji haina budi kufanya
ufuatiliaji ili kubaini iwapo wafugaji hao wanaishi nchini kwa kufuata sheria
Katika mkutano wa bunge uliomalizika mwezi Februari mwaka
huu , wabunge wa mkoa huo kupitia kauli
ya mbunge wa Muleba kaskazini charles Mwijage na Mbunge wa Karagwe Godbes
waliitaka serikali kutoa tamko lini wahamiaji haramu na walio na mifugo
wataondoka mkoani kagera kwa kuwa wanaharibu mazingira na kuhatarisha usalama
wa raia na mali zao
Waziri wa mambo ya ndani Shamsi Vuai Nahodha aliahidi kuchukua hatua dhidi ya
watu wanaodaiwa kuingiza mifugo kutoka nchi jirani na kusababisha madhara
mbalimbali mkoani humo baada ya kutoa agizo kwa kamati za ulinzi na usalama za
wilaya zote kuacha kutoa vibali kwa
wahamiaji hao kupitia ngazi yoyote .
Kw amuda mrefu serikali imekuwa ikitoa ahadi za kuwaondoa
wafugaji hao, kila mara ambapo mwaka
2006 Rais Jakaya Kikwete aliagiza kuondolewa kwa wafugaji hao, lakini agizo
hilo limeshindwa kutekelezwa

No comments:
Post a Comment