Jamii wilayani karagwe na mkoa wa kagera kwa ujumla imetakiwa kuachana na mila na destuli potofu ambazo zinachochea unyanyasaji kwa wanawake.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Afisa ustawi wa jamii bw LAZARO MAJETA amesema kuwa kuna baadhi ya jamii hapa wilayani karagwe ambazo bado zinakumbatia dhana na mila potofu kwakudai kuwa wanawake hawana sauti yeyote ya kudai haki zao au kutoa maoni ambayo yanaweza kuchangia katika suala zima la kimaendeleo .
Hata hivyo bw MAJETA ameeleza kuwa wanawake wamekuwa wakinyanyasika sana katika jamii kwani hawapewi vipau mbele kama ilivyo kwa wanaume akivitaja kuwa ni ukosefu wa elimu pia ushirikishwaji katika masula mbalimbali hususani katika kumiliki ardhi na mashamba hata mali pindi wanapokuwa wameondokewa na waume zao.
Aidha bw MAJETA hakusita kuzungumzia suala la mahari katika jamii na kusema kuwa suala hilo limepelekea wanawake wengi kunyanyasika katika jamii na hata katika familia zao kwa ujumla kwani wanapotolewa mahari waume zao wanawatumia kama wapendanyo kwa kudai kuwa amemnunua kwa hiyo atamnyanyasa awezavyo .
Sanjari na hayo bw MAJETA amewataka wanajamii wote kujua na kutambua kuwa haki za mwanamke ni haki za binadamu na hivyo basi jamii haina budi kuwathamini na kuongeza kuwa iadara yake imejipanga kuwa chukulia hatua watu wote ambao wanawanyanyasa wanawake.
Baadhi ya wnafunzi wilayani karagwe mjini kayanga wametaja changamoto mbalimbali wanazokumbanaa nazo wanapopata mamba wakiwa shule
No comments:
Post a Comment