Na Juhudi Felix
karagwe
karagwe
Mkuu wa Mkoa wa Kagera Kanali mstaafu Fabian Massawe
ameiagiza kampuni ya ujenzi CMG CONSTRUCTION CO.LTD inayoendelea na ujenzi wa mradi wa umwagiliaji
Bujuruga ulioko katika kata ya Bugene Wilayani Karagwe kuhakikisha inakamilisha mradi huo Kabla ya
mwezi Aprili la sivyo mkandarasi atalipa fidia kwa Serikali
Alitoa agizo hilo juzi wakati alipofanya ukaguzi wa mradi na
kupewa taarifa na mkandarasi wa Halmashauri ya Wilaya hiyo Baraka Sanga kuwa mradi
huo ulitegemewa kumalizika Februari mwaka huu lakini mpaka hivi sasa ni asilimi
30 tu ya mradi ndio imekamilika.
“ Sawa yameishatokea inavyoonekana hamataweza kumaliza kwa muda uliopangwa kwahiyo naagiza katika
miezi miwili ijayo asilimia 70 ya mradi iliyobaki iwe imekamilika kama sio sisi
tutaanza kukata faida ambapo mtakuwa mkitulipa asilimi 18 kila mwezi
kwenye milioni 580 mnazopaswa kulipwa,mwezi wa nne mwishoni mnatakiwa muwe
mmekabidhi ,tumewaongezea muda pengine mlikwama kutokana na mambo madogo madogo
kama vile mvua lakini pamoja na hayo angalia vifaa mnavyotumia vimezeeka mnatakiwa
kuongeza nguvu kakodishe vifaa
vinavyoweza kufanya kazi hata kwa wachina mmekuja kufanya kazi hapa”alisema
kanali Masawe kwa ukali.
Alisema lengo la Serikali ni kuhakikisha wakulima
wananufaika kupitia kilimo cha umwagiliaji kwa kulima kilimo chenye tija na sio
cha kuchumia tumbo kwa hiyo Halmashauri ya Wilya ya Karagwe ilitenga milioni
580 ili kuanzisha ujenzi wa mradi wa umwagiliaji ambao unatarajiwa kuhudumia zaidi ya kaya 300
za kata ya Bugene zinazotegemea kuanzisha kilimo cha mpunga na mazao mengine.
Wakati huo huo katiika taarifa ya mradi iliyosomwa na katibu
w amradi huo Fard Hamad kwa niaba ya kamati mbele ya mkuu wa mkoa Massawe
alibainisha kuwa wananchi walioko katika
eneo la mradi huo wanaidai kampuni hiyo kiasi cha shilingi milioni kumi
kutokana na huduma mbalimbali walizozitoa kwa wafanyakazi wa kampuni hiyo
zikiwemo chakula na nyumba za kupanga.
Wananchi hao katika Taarifa hiyo wamemuomba mkuu wa mkoa
kuagiza mkandarasi huyo aweze kuwalipa deni la hilo lililodumu kwa zaidi ya
miezi minane ili waweze kurudisha mtaji wao na kuendeleza biashara zao.
Kwa upande wa mkandarasi wa Halamashauri ya Karagwe Baraka
Sanga alisema kuwa mkandarasi aliyepewa
kazi hiyo hana wasimamizi wazuri “unaweza kuona mkandarasi anayepaswa
kuwepo hapa hayupo anawaachia washauri hawajui kazi hii vizuri ,yeye anaacha
washauri ambao hawana uzoefu na kazi hii mfano aliwaachia
watu hawa anaodai kuwa ni makandarasi wajenga wia wakajenga tofauti na mchoro
tulipokagua tukawataka wabomoe na kujenga upya kwa kufuata mchoro kwahiyo hari hiyo
inatupa taabu pia imechangia mradi kuto kamilika kwa kati”aliongeza Sanga
Kwa upande wa Mhandisi
Marco Mkenda wa kampuni hiyo inayolalamikiwa kutokamilisha mradi kwa
wakati na kuwatapeli wananchi kiasi cha shilingi milioni 10 alisema kuwa baada
ya mkubwa wake aliyepo Dar es Salaam kupata malalamiko hayo aliamua kumtuma
yeye ili aje kutatua tatizo hilo ili mradi uweze kukamalika mapema kama ilivyo
pangwa.
“Baada ya bosi makao makuu Dar kupata malalamiko hayoa
alinituma nije nione kuna nini ndipo iligundulika kuwa mwenzetu aliyetangulia
alipewa pesa ya ujenzi akaitumia visivyo na hata hiyo inayodaiaw ana vibarua
pamoja na watoa huduma ila sio kiasi cha milioni 10”alisema Mkenda
Massawe ameagiza kamati ya mradi kukaa na mkandarasi huyo
ili kutathimini madeni hayo kisha Halmashauri hiyo ifanye utaratibu wa kuwalipa
wadai hao kutoka katika pesa ya mkandarasi huyo pindi atakapo maliza kazi ili
kuondoa kero hiyo inayopelekea kuwagawa wananchi na wakandarasi wanaokuja
kufanya kazi katika maeneo yao kwa kukosa imani nao.
Amemtaka afisa kilimo wa Wilaya na timu yake kuwaelimisha
wakulima juu ya kilimo cha umwagiliaji kupitia mashamba darasa kwani katika
Wilaya hiyo ni mara ya kwanza kujihusisha na kilimo cha huku akiwataka wananchi kuwa karibu na
wakandarasi ili waone mradi unavyoendelea ili waweze kuhoji pale penye
mapungufu kupitia kamati ya miradi
No comments:
Post a Comment